Makundi ya kigaidi yanayoungwa mkono na nchi za kigeni yameshambulia hospitali na maeneo kadhaa ambayo yako chini ya udhibiti wa serikali katika mji wa Aleppo, kaskazini mwa Syria na kusababisha mauaji ya watu wasiopungua 19.
Takwimu za hivi punde za Umoja wa Mataifa zinaonyesha kuwa idadi ya watu waliouawa katika machafuko na wimbi la mashambulizi ya kigaidi nchini Iraq mwezi uliopita wa Aprili ni watu 741.
Kwa akali watu 38 wameuawa na wengine 86 kujeruhiwa katika mashambulizi pacha ya mabomu ya kutegwa kwenye magari katika mji wa Samawa, kusini mwa Iraq.
Kundi la kigaidi na kitakfiri la al-Shabaab limeua askari 15 wa jeshi la Somalia sanjari na kuchukua udhibiti wa mji wa Runirgood, yapata kilomita 180 kaskazini mashariki mwa mji mkuu Mogadishu.
Kwa akali watu 12 wameuawa na makumi ya wengine kujeruhiwa katika mashambulizi mawili ya bomu katika mji mkuu wa Iraq, Baghdad.
Makumi ya watu wameuawa na mamia ya wengine kujeruhiwa katika mripuko wa bomu ulioutikisa mji wa Kabul karibu na ubalozi wa Marekani nchini Afghanistan mapema leo.
Rais John Dramani Mahama wa Ghana ameamuru kuchukuliwa hatua kali za kiusalama baada ya kuongezeka wimbi la mashambulizi ya kigaidi katika nchi za magharibi mwa Afrika.
Spika wa Majilisi ya Ushauri ya Kiislamu yaani Bunge la Iran amesema ukosefu wa usalama na wimbi la mashambulio ya kigaidi katika Ulimwengu wa Kiislamu vinafanywa na wale wanaotumikia maslahi ya utawala wa kizayuni wa Israel.
Kundi la kigaidi la Daesh limetuma wanachama 400 katika nchi za Ulaya kwa ajili ya kufanya mashambulizi ya kigaidi.