-
Serikali ya Somalia yapinga kuingiliwa katika masuala yake ya ndani
Apr 17, 2018 03:35Rais Mohamed Abdullahi Mohamed wa Somalia amesema kuwa, serikali na wananchi wa nchi hiyo wanapinga uingiliaji wa madola ya kigeni katika masuala ya ndani ya nchi hiyo
-
Maelfu ya watu wakimbia makazi yao Ethiopia
Apr 16, 2018 09:50Maelfu ya watu wamelazimika kukimbia makazi yao katika maeneo ya mpaka wa Ethiopia na Somalia kutokana na mapigano makali yanayoendelea katika eneo hilo.
-
Uhusiano wa Somalia na Umoja wa Falme za Kiarabu wazidi kuzorota
Apr 15, 2018 12:13Mzozo katika uhusiano baina ya Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) na Somalia umezidi kuzorota kutokana na hatua ya Imarati kuingilia mambo ya ndano ya nchi hiyo.
-
Watu watano wauawa kwa mripuko wa bomu katika uwanja wa mpira Somalia
Apr 13, 2018 00:12Kwa akali watu watano wameuawa katika shambulio la kigaidi la mripuko wa bomu ulilotokea katika uwanja wa mpira wa miguu, kusini mwa Somalia.
-
Hatimaye Spika wa Bunge la Somalia ajiuzulu
Apr 09, 2018 02:51Spika wa Bunge la Federali la Somalia, Mohamed Sheikh Osman Jawari, hatimaye amejiuzulu baada ya nchi hiyo ye Pembe ya Afrika kushuhudia taharuki na mgogoro mkubwa wa kisiasa kwa wiki kadhaa.
-
AMISOM: Hatutahusika kwa namna yoyote katika mgogoro wa kisiasa nchini Somalia
Apr 07, 2018 11:43Kikosi cha Askari wa Kulinda Amani cha Umoja wa Afrika AU nchini Somalia AMISOM kimetoa taarifa kikikanusha kuhusika kwa namna yoyote katika mkwamo wa kisiasa wa hivi sasa ndani ya serikali ya nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.
-
Watu 6 wauawa katika shambulizi la bomu Mogadishu, Somalia
Apr 07, 2018 03:23Kwa akali watu sita wameuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa kufuatia milipuko pacha ya mabomu iliyotokea katika mji mkuu wa Somalia, Mogadishu jana Ijumaa.
-
Askari wa Uganda waua magaidi 22 wa Al-Shabaab nchini Somalia
Apr 02, 2018 03:09Jeshi la Uganda UPDF limesema askari wake walio katika Kikosi cha Kulinda Amani cha Umoja wa Afrika Somalia, AMISOM, wamewaua magaidi 22 wa kundi la al-Shabab.
-
Al Shabab yashambulia kambi ya Umoja wa Afrika karibu na Mogadishu
Apr 01, 2018 12:54Wanamgambo wa kundi la al Shabab leo wamepigana kwa masaa kadhaa na wanajeshi wa Umoja wa Afrika baada ya kulipua gari walilotega bomu ndani yake nje ya kambi ya wanajeshi hao.
-
Rais wa Somalia asimamisha kikao cha kumuuzulu Spika wa Bunge
Apr 01, 2018 03:09Rais Mohammed Abdullahi Farmajo wa Somalia jana alilazimika kusimamisha kikao cha Bunge la Federali la nchi hiyo kilichokusudia kumuengua madarakani Spika wa bunge hilo.