-
Wanamgambo wa kikoo kuingizwa katika Jeshi la Somalia
Mar 31, 2018 10:31Vikosi vya Umoja wa Afrika vya kulinda Amani nchini Somalia, maarufu kama AMISOM, vimetangaza kuanza kwa zoezi la kuwasajili kwa njia ya kielektroniki wapiganaji wa makundi ya wanamgambo wa kikoo katika eneo la Jubbaland, ikiwa ni mchakato wa kuwajumuisha katika jeshi la serikali katika jimbo hilo.
-
Ujenzi wa ukuta katika mpaka wa Kenya na Somalia wasimamishwa
Mar 30, 2018 10:38Shughuli ya kujenga ukuta wa kilomita 700 katika mpaka wa Kenya na Somalia imesimamishwa kwa muda, ili kutoa nafasi ya kufanyika mashauriano zaidi kati ya nchi mbili hizo jirani.
-
Somalia yaitaka UN kusitisha uvamizi wa Imarati Somaliland
Mar 29, 2018 00:04Mwakilishi wa Somalia katika Umoja wa Mataifa amelaani hatua ya Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) ya kukiuka maazimio ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na ametaka hatua za lazima zichukuliwe ili kusitisha uchokozi huo wa Imarati.
-
Marekani yamzuia rais wa zamani wa Somalia kuingia nchini humo
Mar 27, 2018 03:13Aliyekuwa rais wa Somalia amenyimwa viza ya kuingia nchini Marekani, chini ya dikrii iliyopasishwa na Rais Donald Trump ya kuzuia watu na wahajiri kutoka nchi za Kiislamu kuingia nchini humo.
-
Mgogoro wa kisiasa nchini Somalia waitia wasiwasi IGAD
Mar 26, 2018 23:03Jumuiya ya Maendeleo ya Kiserikali ya Nchi za Afrika Mashariki IGAD imeeleza wasiwasi iliyonao juu ya kushtadi mgogoro wa kisiasa nchini Somalia.
-
Watu 14 wauawa katika mlipuko wa bomu Mogadishu, Somalia
Mar 23, 2018 00:02Kwa akali watu 14 wameuawa na makumi ya wengine kujeruhiwa kufuatia mlipuko wa bomu uliotokea katika mji mkuu wa Somalia Mogadishu.
-
Jumuiya ya IGAD yataka kuhitimishwa mgogoro wa wakimbizi Somalia
Mar 22, 2018 23:29Jumuiya ya Maendeleo ya Kiserikali ya Nchi za Afrika Mashariki IGAD imesisitiza tena uungaji mkono wake wenye lengo la kuhitimisha mgogoro wa wakimbizi nchini Somalia.
-
AU: Mamlaka za ndani Somalia ziimarishe vita dhidi ya al-Shabaab
Mar 14, 2018 10:55Mjumbe wa ngazi za juu wa Umoja wa Afrika nchini Somalia ameyataka maeneo yenye mamlaka ya ndani katika nchi hiyo ya Pembe ya Afrika yaimarishe makabiliano dhidi ya kundi la kigaidi na la kitakfiri la al-Shabaab.
-
Bunge la Somalia lapinga makubaliano ya Imarati na Somaliland
Mar 13, 2018 04:05Bunge la Federali la Somalia limepiga kura kwa kishindo kupinga makubaliano ya pande tatu kati ya eneo la Somaliland, Umoja wa Falme za Kiarabu na Ethiopia kuhusu bandari ya Berbera, iliyoko katika Ghuba ya Aden.
-
Askari wanne wa Somalia wauawa katika shambulio la bomu karibu na Mogadishu
Mar 11, 2018 03:48Askari wasiopungua wanne wa vikosi vya usalama vya Somalia wameuawa na mwengine mmoja amejeruhiwa katika mripuko wa bomu uliotokea kwenye viunga vya mji mkuu wa nchi hiyo Mogadishu.