-
Umoja wa Mataifa walaani shambulizi la kigaidi na mauaji ya waziri Mogadishu
Jun 28, 2016 09:39Mwakilishi maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia, Michael Keating, amelaani vikali shambulizi la kigaidi lililotokea mwishoni mwa wiki iliyopita dhidi ya hoteli ya Naso Hablod kusini mwa Mogadishu, ambako watu 25 waliuawa na wengine wengi kujeruhiwa.
-
Shambulio la kigaidi nchini Somalia
Jun 26, 2016 06:20Shambulio la kigaidi la wanamgambo wa al-Shabab dhidi ya hoteli moja katika mji mkuu wa Somalia Mogadishu kwa mara nyingine tena limepelekea zaidi ya watu 40 kuuawa na kujeruhiwa.
-
Uganda yatangaza tarehe ya kuondoa askari wake Somalia
Jun 24, 2016 09:56Uganda imetangaza kuwa itaondoa askari wake walioko nchini Somalia chini ya mwavuli wa Kikosi cha Kusimamia Amani cha Umoja wa Afrika AMISOM kufikia mwishoni mwa mwaka ujao 2017.
-
Dunia yaipongeza Kenya kwa kupunguza uharamia Afrika Mashariki
Jun 18, 2016 09:25Hatua ya Kenya kutuma jeshi lake nchini Somalia imechangia kupunguza kwa kiasi kikubwa uharamia katika pwani ya Bahari ya Hindi Afrika Mashariki.
-
Viongozi wa Somalia wakasirishwa na misaada ya chakula ya UN ya nafaka zilizooza
Jun 17, 2016 00:14Viongozi wa Somalia wamekasirika kwa kutumwa nchini humo misaada ya chakula ya Umoja wa Mataifa ya nafaka zilizooza kwa ajili ya raia wa nchi hiyo.
-
UNHCR: Muda zaidi unahitajika kuwahamisha wakimbizi Wasomali nchini Kenya
Jun 13, 2016 22:39Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) Filippo Grandi, amesema serikali ya Kenya inapaswa kulegeza msimamo wake kuhusu muda wa mwisho iliotoa kwa ajili ya kuwarejesha makwao wakimbizi wapatao 350,000 Wasomali walioko nchini humo.
-
Mkuu wa UNHCR azuru Kenya kujadili kurejeshwa nyumbani wakimbizi kutoka Somalia
Jun 10, 2016 09:50Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuwahudumia Wakimbizi UNHCR Filippo Grandi yuko nchini Kenya ili kutathmini hali ya kambi ya wakimbizi ya Dadaab baada ya Kenya kuchukua uamuzi wa kufunga kambi hiyo yenye wakimbizi kutoka Somalia.
-
AMISOM yaangamiza wanachama 110 wa al-Shabaab Somalia
Jun 09, 2016 09:40Kikosi cha Kulinda Amani cha Umoja wa Afrika nchini Somalia AMISOM kimesema askari wake wamefanikiwa kuangamiza makumi ya wanachama wa kundi la kigaidi na kitakfiri la al-Shabaab walipojaribu kushambulia moja ya kambi zao.
-
Somalia: Tuko tayari kuwapokea wakimbizi wa Dadaab
Jun 08, 2016 09:55Rais Hassan Sheikh Mohamoud wa Somalia amesema nchi yake iko tayari kuwapokea raia wake kutoka kambi ya ya wakimbizi ya Dadaab nchini Kenya, kwa shabaha ya kuwapa fursa wakimbizi hao kujenga taifa lao.
-
Askari wa AMISOM wakamatwa kwa kuuza bidhaa za kikosi hicho
Jun 07, 2016 03:03Kikosi cha Kulinda Amani cha Umoja wa Afrika nchini Somalia AMISOM kinawazuilia askari wake watano wanaotuhumiwa kuuza kinyume cha sheria suhula na bidhaa za kikosi hicho.