-
UN: Zaidi ya watu 13,000 wameuawa katika vita vya Sudan
Jan 22, 2024 03:59Zaidi ya watu 13,000 wameuawa na wengine 26,000 kujeruhiwa katika vita vinavyoendelea nchini Sudan tangu mwaka jana, ofisi ya Umoja wa Mataifa ya masuala ya kibinadamu imetangaza Jumapili.
-
Mapigano ya kikabila yameua zaidi ya 15,000 katika mji mmoja Sudan
Jan 20, 2024 03:51Ripoti ya Umoja wa Mataifa imesema watu kati ya 10,000 na 15,000 waliuawa katika ghasia na mapigano ya kikabila mwaka jana katika mji mmoja ulioko katika jimbo la Darfur Magharibi nchini Sudan.
-
Ethiopia na Sudan zasusia mkutano wa Jumuiya ya IGAD
Jan 18, 2024 07:22Ethiopia imesema mkutano wa Wakuu Jumuiya ya Maendeleo ya Kiserikali (IGAD) umefanyika leo Alhamisi huku ikiwa na mipango mengine. Wakati huo huo Sudan pia imedai kuwa haikushirikishwa katika ajenda ya mkutano huo.
-
Vita vya Sudan vyapanuka hadi katika mabaki ya ufalme wa kale wa Kush
Jan 17, 2024 23:24Vita vikali vya miezi tisa huko Sudan kati ya majenerali wawili hasimu vimepanuka zaidi hadi kwenye eneo la Urithi wa Dunia wa Shirika la UNESCO. Hii ni kwa mujibu wa ripoti ya shirika lisilo la kiserikali la The Regional Network for Cultural Rghts.
-
Sudan 'yasimamisha' ushirikiano na jumuiya ya IGAD
Jan 16, 2024 23:05Wizara ya Mambo ya Nje ya Sudan imetangaza kusimamisha ushirikiano na Jumuiya ya Maendeleo ya Kiserikali (IGAD), hatua ambayo wadadisi wa mambo wanasema inaashiria kugonga mwamba jitihada za hivi punde za kieneo za kuhitimisha vita katika nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika.
-
Kadhaa wauawa Abyei mpakani mwa Sudan na Sudan Kusini
Jan 01, 2024 08:50Kwa akali watu sita wameuawa katika shambulizi linaloamini ni la ulipizaji kisasi katika eneo linalozozaniwa la Abyei, kwenye mpaka wa Sudan na Sudan Kusini.
-
Kusimamishwa shughuli za Madaktari Wasio na Mipaka huko Al-Jazīrah, Sudan
Dec 31, 2023 03:51Shughuli za Madaktari Wasio na Mipaka zimesitishwa katika Jimbo la Al Jazirah nchini Sudan kutokana na kuendelea kuwa mbaya hali ya usalama katika jimbo hilo.
-
Kiongozi wa RSF yuko Addis Ababa baada ya kushindwa kukutana na Al-Burhan
Dec 28, 2023 22:59Kamanda wa wapiganaji wa Kikosi cha Msaada wa Haraka kinachopigana na jeshi la Sudan, Luteni Jenerali Mohamed Hamdan Dagalo, aliwasili katika mji mkuu wa Ethiopia, Addis Ababa, jana Alhamisi baada ya kutembelea Uganda na kukutana na Rais Yoweri Museveni.
-
"Save Sudan"... Kampeni kuu kwenye mitandao ya kijamii ikiangazia yanayojiri nchini humo
Dec 21, 2023 23:36Wanaharakati wa mitandao ya kijamii wameanzisha kampeni kubwa iliyopewa jina la Save Sudan inayoangazia na kumulika masaibu yanayowapata wananchi wa Sudan kutokana na mapigano yanayoendelea nchini humo na kupuuzwa na jamii ya kimataifa hasa vyombo vya habari ambavyo aghlabu vimeelekeza mazingatio yao huko Gaza na mauaji ya raia wa Palesrina yanayofanywa na Israel.
-
WFP yasimamisha usambazaji wa chakula Sudan, mapigano yaenea
Dec 21, 2023 07:53Mpango wa Chakula Dunia (WFP) umesimamisha kwa muda utoaji na usambazaji wa chakula katika baadhi ya maeneo katika jimbo la al-Jazira katikati ya Sudan, huku mapigano yakipanuka na kuenea pande za mashariki na kusini mwa mji mkuu wa nchi hiyo, Khartoum.