-
Askari wa China watumwa Sudan kulinda amani
Dec 11, 2018 15:34Askari 100 wa kulinda amani wa China wameondoka Jumanne ya leo Beijing kuelekea Darfur, nchini Sudan kwa ajili ya majukumu ya kulinda amani kwa kipindi cha mwaka mmoja katika kikosi cha Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika (UNAMID).
-
Viongozi wa Sudan Kusini watoa mwito kwa wananchi kusameheana
Dec 08, 2018 15:33Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir na naibu wake Wani Igga wanaendeleza kampeni ya pamoja wakitaka kuwaunganisha na kuwapatanisha watu wa Sudan Kusini waliosambaratika kutokana na vita vikali vya miaka mitano.
-
Umoja wa Mataifa walaani wimbi la mashambulizi ya kinyama ya kingono Sudan Kusini
Dec 03, 2018 01:09Umoja wa Mataifa jana Jumapili ulilaani wimbi la mashambulizi ya kinyama ya kingono dhidi ya wanawake na mabinti katika mji wa Bentiu kaskazini mwa Sudan Kusini yaliyojiri katika eneo linalotajwa kuwa lililo chini ya udhibiti wa serikali.
-
Sudan Kusini yakanusha kukiuka marufuku ya usafirishaji silaha
Nov 30, 2018 06:59Sudan Kusini imekanusha tuhuma kuwa nchi jirani yake Uganda inaisaida kupata silaha za Ulaya licha ya vikwazo vya silaha vilivyowekwa na Umoja wa Ulaya.
-
Uganda iliisadia Sudan Kusini kukiuka vikwazo vya silaha vya EU
Nov 29, 2018 13:35Kundi moja la kudhibiti silaha leo limeeleza kuwa Uganda ilisaidia kuingiza nchini Sudan Kusini silaha na zana za kijeshi za Ulaya wakati wa vita vya ndani nchini humo na hivyo kukiuka vikwazo vya silaha vya Umoja wa Ulaya dhidi ya nchi hiyo.
-
Vyama vya siasa Sudan vyapinga kuwepo uhusiano na utawala haramu wa Israel
Nov 26, 2018 04:33Vyama vya siasa nchini Sudan vimetoa wito wa kupambana na hatua zinazofanywa na baadhi ya nchi za Kiarabu za kutaka kuanzishwa uhusiano na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
UN: Mapatano ya amani ya Sudan Kusini ni legelege
Nov 17, 2018 16:14Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya amani ametahadharisha kuwa, makubaliano ya amani ya Sudan Kusini ni tete na legelege na ni sawa na kuhifadhi fedha taslimu.
-
Watu 15 wameuawa katika mapigano ya kikabila nchini Sudan Kusini
Nov 03, 2018 14:27Watu 15 wameuawa na wengine 20 kujeruhiwa katika mapigano ya kikabila yaliyodumu kwa siku tatu mfululizo mkoani Jonglei, Sudan Kusini.
-
Sudan Kusini yawaachia huru msemaji na mshauri wa kiongozi wa waasi
Nov 02, 2018 16:06Sudan Kusini leo imewaachia huru kutoka jela msemaji na mshauri wa Riek Machar kiongozi wa waasi wa nchi hiyo. Hayo yameelezwa na afisa wa serikali ya Juba.
-
Kiongozi wa waasi Sudan Kusini arejea nchini baada ya kufikiwa makubaliano ya amani
Oct 31, 2018 15:43Riek Machar kiongozi wa waasi Sudan Kusini leo Jumatano amewasili Juba mji mkuu wa nchi hiyo kuadhimisha makubaliano ya amani; ikiwa imepita zaidi ya miaka miwili baada ya kuibuka mapigano makali huko Juba na kumlazimisha kukimbia nchi.