-
UN yaonya juu ya hali mbaya ya kibinaadamu nchini Sudan Kusini
Aug 11, 2016 08:53Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anayeshusika na Uratibu wa Masuala ya Kibinaadamu na Misaada ya Dharura ameonya juu ya ukosefu wa makazi na ukame huko nchini Sudan Kusini.
-
UN yakaribisha hatua ya Juba kukubali kutumwa askari wa kikanda
Aug 08, 2016 03:19Umoja wa Mataifa umepongeza hatua ya Sudan Kusini kukubali pendekezo la kutumwa askari wa kieneo nchini humo kufuatia mapigano ya ndani kati ya askari watiifu kwa Rais Salva Kiir na wafuasi wa aliyekuwa makamu wake, Riek Machar.
-
Sudan Kusini yakubali kutumwa askari wa kieneo nchini
Aug 06, 2016 02:25Serikali ya Sudan Kusini imekubali pendekezo la jumuiya ya kieneo ya IGAD la kutumwa askari wa kulinda amani nchini humo, suala ambalo awali lilikuwa limepingwa vikali na Rais Salva Kiir wa nchi hiyo.
-
UN: Maafisa usalama Sudan Kusini wameua na kubaka
Aug 04, 2016 10:37Umoja wa Mataifa umeitaka serikali ya Sudan Kusini kuwachukulia hatua za kisheria maafisa usalama walioua raia na kunajisi wanawake na mabinti wadogo katika machafuko ya mwezi uliopita katika mji mkuu Juba.
-
Makumi wapoteza maisha katika mafuriko makali nchini Sudan
Aug 04, 2016 03:31Makumi ya watu wameripotiwa kupoteza maisha yao katika mafuriko makubwa yaliyoikumba mikoa 13, kufuatia kunyesha mvua kali nchini humo.
-
Rais wa Sudan Kusini awapiga kalamu nyekundu mawaziri sita wa Machar
Aug 03, 2016 09:30Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amewapiga kalamu nyekundu mawaziri sita wa upande wa makamu wake wa zamani wa rais yaani Riek Machar.
-
UNHCR: Maelfu wamekimbia machafuko Sudan Kusini
Aug 02, 2016 21:53Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR) limetangaza kuwa maelfu ya watu wamekimbia machafuko na mapigano mapya yaliyozuka nchini Sudan Kusini huku kukiripotiwa matukio ya mauji ya umati, uporaji na watoto wadogo kushirikishwa vitani kwa nguvu.
-
Kuzidi kuwa mbaya hali ya mambo huko Sudan Kusini
Aug 02, 2016 11:57Mwenyekiti wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa amesema kuwa, hali ya mambo katika mji mkuu wa Sudan Kusini Juba imezidi kuwa mbaya.
-
Waziri mashuhuri wa upande wa upinzani Sudan Kusini ajiuzulu
Aug 02, 2016 11:14Waziri mashuhuri wa serikali ya Sudan Kusini kutoka upande wa upinzani amejiuzulu wadhifa wake, hatua iliyotajwa kuwa ni pigo kubwa kwa makubaliano ya amani yanayolegalega ya nchi hiyo.
-
Waziri: Makubaliano ya amani Sudan Kusini yamevunjika
Aug 02, 2016 02:54Mgogoro wa kisiasa nchini Sudan Kusini umechukua mwelekea mpya baada ya Waziri wa Kilimo wa nchi hiyo kutoka upande wa upinzani kujiuzulu na kusisitiza kuwa makubaliaono ya amani yaliyosainiwa na pande mbili yamevunjika.