-
Wananchi wa Tunisia waandamana kulaani mapatano ya Imarati na utawala wa Kizayuni
Aug 23, 2020 21:58Wananchi wa Tunisia wamefanya maandamano makubwa kupinga mapatano yaliyofikiwa kati ya Imarati na utawala wa Kizayuni wa Israel ya kuanzisha uhusiano wa kidiplomasia kati ya pande mbili hizo.
-
Bunge la Tunisia limelaani mapatano kati ya Imarati na utawala wa Kizayuni
Aug 18, 2020 02:27Bunge la Tunisia limelaani mapatano yaliyofikiwa ya kuanzisha uhusiano wa kidiplomasia kati ya Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) na utawala ghasibu wa Israel.
-
Rais wa Tunisia: Msingi wa mirathi katika Uislamu ni uadilifu na insafu
Aug 17, 2020 03:08Rais Kais Saied wa Tunisia ameamsha hasira za jumuiya za wanawake za kiliberali baada ya kusisitiza kwamba msingi wa mirathi katika dini ya Uislamu ni uadilifu na insafu na kwamba suala hilo limeshapewa ufumbuzi katika aya za Qu'ani tukufu ambao hauhitajii tena tafsiri wala taawili.
-
Waziri Mkuu mteule wa Tunisia: Nitaunda serikali ya mateknokrati watupu
Aug 11, 2020 06:50Waziri Mkuu mteule wa Tunisia amesema kuwa ataunda serikali ya mateknokrati watupu bila ya kuvishirikisha vyama vingine kufuatia mivutano iliyopo baina vyama vya siasa kuhusu uundaji wa serikali mpya nchini humo.
-
Spika wa Bunge la Tunisia asisitiza ushirikiano zaidi na Uturuki
Aug 02, 2020 22:59Spika wa Bunge la Tunisia amefanya mazungumzo na mwenzake wa Uturuki ambapo ametoa wito wa kuimarishwa uhusiano wa nchi hizo mbili.
-
Spika wa Bunge la Tunisia aponea chupuchupu kuuzuliwa
Jul 30, 2020 21:57Spika wa Bunge la Tunisia ameponea chupuchupu kupigiwa kura ya kutokuwa imani naye baada ya wabunge wanaompinga kushindwa kutimiza idadi ya kura 107 zilizohitajika ili kuweza kumuuzulu wadhifa huo.
-
Tunisia yaiunga mkono Serikali ya Mwafaka wa Kitaifa nchini Libya
Jul 29, 2020 22:48Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya Tunisia imetangaza kuwa, nchi hiyo itaendelea kuiunga mkono Serikali ya Mwafaka wa Kitaifa ya Libya.
-
Waziri Mkuu mpya ateuliwa nchini Tunisia
Jul 26, 2020 20:59Kufuatia kuendelea mgogoro wa kisiasa nchini Tunisia baada ya kujiuzulu Waziri Mkuu Elyes Fakhfakh, rais wa nchi hiyo Kais Saied, amemteua waziri wa mambo ya ndani Hichem Mechichi kuwa waziri mkuu mpya na kumtaka aunde baraza jipya la mawaziri.
-
Waziri Mkuu wa Tunisia ajiuzulu na kuitumbukiza nchi katika mgogoro wa kisiasa
Jul 15, 2020 23:23Waziri Mkuu wa Tunisia ametangaza kujiuzulu, hatua ambayo imeitumbukiza nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika katika mgogoro mwingine wa kisiasa.
-
Iran na Tunisia zatilia mkazo ulazima wa kustawishwa ushirikiano wa pande mbili
Jul 07, 2020 06:33Balozi wa Iran nchini Tunisia amefanya mazungumzo na waziri wa biashara wa nchi hiyo na pande mbili zimejadiliana njia za kuimarisha na kustawisha uhusiano wa pande mbili hasa wa kiuchumi.