Maelfu ya Waisraeli wamemiminika mabarabarani kwa wiki ya tano mfululizo kushiriki maandamano ya kushinikiza kufungwa jela Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni, Benjamin Netanyahu kutokana na kashfa za ufisadi wa kifedha zinazomuandama.
Cyril Ramaphosa kiongozi mpya wa chama tawala nchini Afrika Kusini ANC amesema leo kuwa ameazimia kukomesha ufisadi na kutekeleza sera ya mageuzi makali ya kiuchumi ambayo yataharakisha utaifishaji wa ardhi bila ya fidia.
Wakazi wa ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu utawala wa Kizayuni wameandamana huko Tel Aviv wakitaka kushughulikiwa kesi ya ufisadi inayomkabili Waziri Mkuu wa utawala huo ghasibu.
Waziri wa Afya na Huduma za Binaadamu nchini Marekani, Tom Price amelazimika kujiuzulu kutokana na kashfa ya ufisadi inayomkabili.
Rais aliyeondolewa madarakani hivi karibuni wa Korea Kusini, Park Geun-hye amekamatwa na polisi ya nchi hiyo kwa tuhuma za ufisadi na utumiaji mbaya wa madaraka.
Waendesha mashtaka nchini Korea Kusini wametoa wito wa kutolewa waranti wa kukamatwa rais aliyeondolewa madarakani hivi karibuni wa nchi hiyo, Park Geun-hye.
Upinzani dhidi ya Benjamin Netanyahu, Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel umeongezeka sana hivi sasa. Mamia ya wakazi wa ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu wanaendelea kuandamana wakimshikinikiza Netanyahu ajiuzulu.
Mamia ya wakazi wa utawala wa Kizayuni wa Israel wamefanya maandamano ya kulaani ufisadi wa kifedha wa viongozi wa utawala huo hususan Benjamin Netanyahu, Waziri Mkuu wa Israel, mjini Tel Aviv.
Shirika la kutetea haki za umma la SID limetangaza kuwa SERIKALI ya Jubilee nchini Kenya imetimiza ahadi moja pekee kati ya 30 ilizotoa kuhusiana na mikakati ya kupambana na ufisadi.
Maelfu ya wananchi wa Mali wameshiriki katika maandamano makubwa ya kuunga mkono makubaliano ya amani na makundi ya wabeba silaha nchini.