-
Jeshi la Uganda lafelisha mashambulio ya al Shabab, laua makamanda
Feb 19, 2016 23:38Wanajeshi wa Uganda wanaoshiriki kwenye operesheni za kijeshi za kikosi cha Umoja wa Afrika AMISOM nchini Somalia wamefanikiwa kuvunja mashambulio mawili ya kundi la kigaidi la al shabab katika kambi za AU kama ambavyo wamefanikiwa pia kuua makamanda wawili wa kundi hilo katika siku chache zilizopita.
-
Polisi Uganda: Besigye ataachiwa huru baada ya kutangazwa matokeo
Feb 19, 2016 11:35Polisi nchini Uganda imesema itaendelea kumzuilia mgombea wa urais kwa tiketi ya chama cha FDC, Dakta Kizza Besigye na kwamba huenda akaachiwa huru hapo kesho baada ya matokeo rasmi ya uchaguzi wa rais na bunge kutangazwa.
-
Mbabazi: Nitaheshimu matokeo kama yatakuwa ya haki
Feb 19, 2016 04:24Waziri Mkuu wa zamani wa Uganda, Amama Mbabazi amesema atakubali matokeo ya uchaguzi endapo kutakuweko uwazi katika mchakato mzima wa kuhesabu kura.
-
Museveni aongoza katika matokeo ya awali ya uchaguzi wa Rais Uganda
Feb 19, 2016 00:08Matokeo ya awali ya uchaguzi wa Rais na Bunge nchini Uganda yanaonyesha kuwa mgombea urais kwa tiketi ya chama tawala cha NRM, Yoweri Kaguta Museveni anaongoza kwa kupata kura nyingi zaidi zilizohesabiwa.
-
Kura zaanza kuhesabiwa Uganda, mitandao ya kijamii yafungwa
Feb 18, 2016 13:12Uchaguzi wa rais na bunge nchini Uganda ambao ulianza saa moja asubuhi leo kwa saa za nchi hiyo katika vituo vingi vya kupiga kura umemalizika saa moja jioni bila kuripotiwa visa vikubwa vya uhalifu na uchakachuaji.
-
AU yawataka raia wa Uganda kuwa watulivu baada ya uchaguzi
Feb 18, 2016 04:49Ujumbe wa waangalizi wa uchaguzi wa Umoja wa Afrika nchini Uganda umetoa wito kwa raia wa nchi hiyo kujitokeza kwa wingi na kutimiza haki yao ya kikatiba ya kuwachagua viongozi wawapendao.
-
Wananchi wa Uganda leo wanashiriki katika uchaguzi wa Rais na Bunge
Feb 17, 2016 23:15Wananchi wa Uganda waliotimiza masharti ya kupiga kura leo wanaelekea katika vituo vya kupigia kura kumchagua Rais na wawakilishi wao wa Bunge.
-
EC yaonya wenye nia ya kuvuruga uchaguzi Uganda
Feb 17, 2016 22:42Tume ya uchaguzi nchini Uganda imewaonya vikali wenye nia ya kuvuruga zoezi la upigaji kura linalofanyika leo (Alkhamisi) na kusisitiza kuwa, watu wa aina hiyo watachukuliwa hatua kali za kisheria. Tume hiyo pia imesisitiza kuwa uchaguzi wa leo nchini Uganda utakuwa huru na wa haki.
-
Paspoti za kielektroniki kuzinduliwa Afrika Mashariki
Feb 17, 2016 03:55Raia wa Nchi za Afrika Mashariki wataanza kutumia paspoti za kielektroniki ambazo zitatumika kurahisisha usafiri kwa wananchi wa eneo hilo.
-
Kampeni zamalizika Uganda, uchaguzi Alkhamisi
Feb 17, 2016 03:33Nchini Uganda kampeni za uchaguzi zilimalizika Jumanne huku wagombea wa viti vya urais na ubunge wakijitayarisha kwa ajili ya upigaji kura siku ya Alkhamisi.