-
UN yashangazwa na wito wa Trump wa kuwatesa na kuwanyanyasa washukiwa
Apr 07, 2017 02:54Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa ameeleza kusikitishwa kwake na wito wa Rais wa Marekani Donald Trump wa kutaka kurejeshwa sheria ya kuwatesa watuhumiwa wa jinai mbalimbali.
-
UN yatahadharisha kuhusu hatari za maharamia wa Somalia
Apr 05, 2017 22:48Mkuu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kupambana na mihadarati na uhalifu ametahadharisha kuhusu hatari, vitisho na mashambulizi ya maharamia wa baharini nchini Somalia.
-
Makaburi mengine 13 ya umati yapatikana katikati ya DRC
Apr 03, 2017 22:59Mkuu wa ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ametangaza habari ya kugunduliwa makaburi mengine mengi ya umati katikati ya nchi hiyo.
-
Umoja wa Mataifa wapinga tena ujenzi wa vitongoji vya walowezi, Palestina
Mar 31, 2017 23:37Msemaji wa Umoja wa Mataifa amesema taasisi hiyo ya kimataifa ina wasiwasi juu ya kuendelezwa ujenzi wa vitongoji vya walowezi wa kizayuni katika ardhi inayokaliwa kwa mabavu ya Palestina.
-
Kamisheni ya Haki za Binadamu yaikosoa Jordan kwa kumkaribisha al Bashir
Mar 31, 2017 23:17Kamisheni Kuu ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa imeikemea serikali ya Jordan kwa kumkaribisha nchini humo Rais Omar Hassan al Bashir wa Sudan anayesakwa na Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC).
-
ICC yatahadharisha kuhusu ukatili unaofanyika Congo DR
Mar 31, 2017 22:52Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) imetahadharisha kuwa ukatili uliofanyika katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ikiwa ni pamoja na mauaji ya wataalamu wawili wa Umoja wa Mataifa unaweza kutambuliwa kuwa ni jinai ya kivita.
-
UN: Idadi ya waliopoteza maisha kutokana na malaria Burundi yapindukia 4000
Mar 29, 2017 22:42Umoja wa Mataifa umesema kuwa, idadi ya watu walioaga dunia kutokana na mripuko wa ugonjwa wa malaria nchini Burundi imeongezeka na kupindukia watu 4000, tangu mwanzoni mwa mwaka huu hadi sasa.
-
Umoja wa Mataifa wawashutumu wanaoeneza uongo kuhusu Uislamu
Mar 29, 2017 09:48Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amewashutumu watu wanaoeneza propaganda chafu dhidi ya Uislamu ambao wanajaribu kuihusisha dini hiyo na vitendo vya kigaidi.
-
Maafisa wawili wa UN waliotekwa nyara Kongo DR, wameuawa
Mar 29, 2017 09:41Imebainika kuwa, maafisa wawili wa Umoja wa Mataifa raia wa Marekani na Sweden waliotekwa nyara katika mkoa wa Kasai katikati ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wiki mbili zilizopita wameuawa.
-
Katibu Mkuu wa UN asikitishwa na mauaji ya wataalamu wawili wa umoja huo nchini Kongo DR
Mar 29, 2017 02:18Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, amesema amesikitishwa na mauaji ya wataalamu wawili wa umoja huo nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.