-
Mamluki wa kundi lenye silaha watiwa mbaroni CAR
Aug 14, 2016 23:13Askari jeshi wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa waliopo Jamhuri ya Afrika ya Kati wametangaza kutiwa mbaroni mamluki kadhaa wa kundi moja lenye silaha nchini humo.
-
Maandamano yashadidi nchini Ethiopia, Umoja wa Mataifa wataka kutumwa waangalizi wa kimataifa
Aug 11, 2016 03:36Maandamano dhidi ya serikali ya Ethiopia yanazidi kushadidi huku serikali ya nchi hiyo ikitumia vyombo vya usalama kuwakandamiza waandamanaji.
-
Israel yamtia mbaroni mwakilishi wa UN Ukanda wa Ghaza
Aug 09, 2016 23:13Utawala wa Kizayuni umemtia mbaroni mwakilishi wa Umoja wa Mataifa katika Ukanda wa Ghaza kwa tuhuma za kuwa na ushirikiano na Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina Hamas.
-
Mwakilishi wa UN asisitiza mgogoro wa Yemen kutatuliwa kwa njia ya mazungumzo
Aug 08, 2016 23:58Ismail Ould Sheikh Ahmed, mwakilishi wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya Yemen amesisitizia kutatuliwa mgogoro wa nchi hiyo kwa njia ya mazungumzo.
-
UN yakaribisha hatua ya Juba kukubali kutumwa askari wa kikanda
Aug 08, 2016 03:19Umoja wa Mataifa umepongeza hatua ya Sudan Kusini kukubali pendekezo la kutumwa askari wa kieneo nchini humo kufuatia mapigano ya ndani kati ya askari watiifu kwa Rais Salva Kiir na wafuasi wa aliyekuwa makamu wake, Riek Machar.
-
Maelfu ya raia wamekuwa wakimbizi kaskazini mwa Kongo
Aug 07, 2016 22:27Ofisi ya Uratibu wa Misaada ya Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa imetangaza kuwa, raia zaidi ya elfu 20 katika wilaya ya Tshopo katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kaskazini mwa nchi hiyo wamekuwa wakimbizi.
-
Iran yaikosoa Magharibi kwa uingiliaji wa masuala ya ndani ya nchi
Aug 06, 2016 03:25Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni wa Iran amekosoa hatua ya nchi za Magharibi ya kuipaka matope Jamhuri ya Kiislamu kwa hatua yake ya kutekeleza hukumu ya kifo dhidi ya magaidi hapa nchini.
-
UN: Maafisa usalama Sudan Kusini wameua na kubaka
Aug 04, 2016 10:37Umoja wa Mataifa umeitaka serikali ya Sudan Kusini kuwachukulia hatua za kisheria maafisa usalama walioua raia na kunajisi wanawake na mabinti wadogo katika machafuko ya mwezi uliopita katika mji mkuu Juba.
-
Wanafunzi Waislamu Ulaya walaani mauaji ya watoto Yemen
Aug 03, 2016 02:55Muungano wa vyama vya wanafunzi wa Kiislamu barani Ulaya umemuandikia barua Ban Ki-moon, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ukitaka hatua za makusudi zichukuliwe kukomesha mauaji ya raia wasio na hatia na hususan watoto wadogo nchini Yemen.
-
Sudan Kusini kuzishawishi UN na IGAD zikubali mabadiliko ya uongozi
Jul 31, 2016 11:49Serikali ya umoja wa kitaifa ya Sudan Kusini imemteua Makamu mpya wa Rais aliyechukua nafasi ya Riek Machar kuufafanulia Umoja wa Mataifa sababu za kufanyika mabadiliko ya uongozi ndani ya chama cha upinzani cha SPLM-IO.