Feb 22, 2019 12:23
Meja Jenerali Qassim Suleimani, Kamanda MKuu wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran SEPAH, amesema kwamba magaidi wa kitakfiri wanaoungwa mkono na Saudi Arabia katika ardhi ya Pakistan wamekuwa tatizo kubwa la usalama kwa majirani wote wa nchi hiyo, zikiwemo India na Afghanistan na kwamba viongozi wa Pakistan wanapasa kulitambua vyema jambo hilo.