Abdul Malik al Houthi, Katibu Mkuu wa harakati ya Answarullah ya Yemen ametangaza kuwa, nchi ambayo hivi sasa inaongoza fikra za Kiwahabi na kuzieneza katika nchi mbalimbali duniani, ni Saudi Arabia.
Katibu Mkuu wa Harakati ya Ansarullah ya Yemen amekosoa vikali misimamo ya Saudi Arabia na mkatakati wake wa kueneza fikra za Uwahabi na kubainisha kwamba, matukio ya kigaidi yanayoshuhudiwa katika maeneo mbalimbali duniani chimbuko lake ni fikra za Kiuwahabi za Saudia.
Serikali ya Ubelgiji imeonyesha wasi wasi wake juu ya kuenea mafundisho ya Uwahabi unaoungwa mkono na utawala wa Saudi Arabia ndani ya nchi hiyo na mataifa mengine ya Ulaya.
Ubelgiji imeeleza wasi wasi wake juu ya kuenea kwa kasi mwangwi wa Uwahabi katika nchi hiyo na kote bara Ulaya kwa ujumla.
Wananchi wa Tunisia hususan tabala la wasomi na wanafikra wa nchi hiyo wamekataa kupokea fikra za kiwahabi licha ya Saudi Arabia kutumia fedha na wakati mwingi kueneza na kusambaza fikra na mitazamo ya kisalafi na kiwahabi katia nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika.
Mshauri Mkuu wa kijeshi wa Amirijeshi Mkuu wa vikosi vya ulinzi vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, uwahabi ambao matunda yake ni makundi ya kigaidi kama vile Daesh na al Qaida, ni maadui wa umoja na uhuru wa nchi za Kiislamu.
Waziri Mkuu wa zamani wa Iraq ametoa wito wa kuwekwa kundi la Kiwahabi katika orodha ya makundi ya kigaidi duniani.
Waislamu wa madhehebu ya Shia huko Nigeria wamekosoa vikali ukandamizaji unaofanywa dhidi yao na vyombo vya usalama nchini humo na kusisitiza kuwa, dhulma hizo zimetokana na fikra za Kiwahabi.
Serikali ya Tunisia imemfuta kazi Waziri wa Masuala ya Dini wa nchi hiyo, baada ya kusema kuwa, idiolojia ya Uwahabi ambayo imetawala Saudi Arabia ndiyo chanzo cha ugaidi duniani.
Mufti katika kasri ya mfalme wa Saudia amesema kusherehekea Maulid ya Mtume Muhammad SAW ni shirki lakini akasema ni wajibu kusherehekea maadhimisho ya kuanza kutawala ukoo wa Aal Saud.