Mashambulizi ya ndege zisizo na rubani za muqawama wa Iraq dhidi ya utawala wa Kizayuni
(last modified Wed, 09 Oct 2024 06:48:03 GMT )
Oct 09, 2024 06:48 UTC
  • Mashambulizi ya ndege zisizo na rubani za muqawama wa Iraq dhidi ya utawala wa Kizayuni

Muqawama wa Kiislamu wa Iraq umelenga shabaha moja muhimu ya utawala habithi wa Kizayuni kusini mwa Palestina inayokaliwa kwa mabavu (Israel).

Muqawama wa Kiislamu wa Iraq umetangaza katika taarifa kuwa, ikiwa ni katika kukabiliana na mauaji na jinai za kinyama zinazofanywa na utawala ghasibu wa Israel dhidi ya raia wakiwemo watoto, wanawake na wazee, wanamapambano wa Kiislamu wa  Iraq wameshambulia shabaha muhimu ya utawala huo katili kwa ndege isiyo na rubani mapema leo Jumatano asubuhi.

Taarifa hiyo pia inasisitiza kuendelea kwa oparesheni za kuponda ngome za adui mzayuni kwa mwelekeo huo huo unaoongezeka kila siku.

Mashambulizi ya ndege zisizo na rubani za wanamapambano wa muqawama wa Kiislamu wa Iraq dhidi ya utawala wa Kizayuni 

Kundi la Muqawama wa Kiislamu la Iraq pia lilitangaza katika taarifa siku ya Jumanne kwamba,  lililenga shabaha tano za Wazayuni katikati na kaskazini mwa ardhi zinazokaliwa kwa mabavu.

Wanamuqawama wa Iraq wamesema walifanya oparesheni hiyo kwa kutumia kombora la  hali ya juu la cruise linalojulikana kama "Al-Aqrab" na ndege isiyo na rubani.

Tangu tarehe 7 Oktoba mwaka uliopita utawala wa Kizayuni umefanya kila aina ya jinai za kivita sambamba na mauaji ya kimbari dhidi ya wananchi wasio na ulinzi wa Palestina huko Ukanda wa Gaza na kuua Wapalestina wapatao 42,000 na kujeruhi wengine zaidi ya 97,000.

Utawala huo unaoua watoto haukuishia katika kufanya jinai za kutisha huko Gaza bali umeeneza jinai hizo kusini mwa Lebanon ambapo umeua zaidi ya raia 2,000 wa nchi hiyo. Mapambano ya muqawama katika nchi za Iraq, Lebanon na Yemen yamejibu vikali mashambulizi hayo ya Kizayuni  na kusimama kidete na kwa  ujasiri mkubwa dhidi ya utawala huo tangu kuanza mashambulizi yake ya kinyama  dhidi ya watu wa Ukanda wa Gaza ili kumlazimisha adui huyo Mzayuni asitishe mashambulizi hayo haraka iwezekanavyo.

Tags