Jeshi la Yemen laangamiza meli ya mizinga ya Saudia, Riyadh yakiri
https://parstoday.ir/sw/news/west_asia-i24495-jeshi_la_yemen_laangamiza_meli_ya_mizinga_ya_saudia_riyadh_yakiri
Jeshi la Yemen Jumatatu ya jana liliangamiza meli ya mizinga ya Saudia na kusababisha makumi ya askari wa nchi hiyo vamizi kuangamizwa na wengine kujeruhiwa.
(last modified 2023-11-27T08:44:11+00:00 )
Jan 31, 2017 01:09 UTC
  • Jeshi la Yemen laangamiza meli ya mizinga ya Saudia, Riyadh yakiri

Jeshi la Yemen Jumatatu ya jana liliangamiza meli ya mizinga ya Saudia na kusababisha makumi ya askari wa nchi hiyo vamizi kuangamizwa na wengine kujeruhiwa.

Sambamba na Saudia kukiri juu ya habari hiyo imedai kuwa, katika shambulizi la jeshi la Yemen dhidi ya meli yake ya mizinga katika pwani ya mkoa wa Al Hudaydah, askari wake wawili waliuawa na wengine watatu kujeruhiwa. Wakati huo huo jeshi la Saudia limeshambulia mji mdogo wa pwani wa Al Mukha kusini mwa mkoa wa Taiz na kusababisha makumi ya raia kuuawa shahidi na wengine wengi kujeruhiwa.

Mfalme wa Saudia anayetekeleza jinai na mauaji dhidi ya raia madhlumu wa Yemen

Aidha shambulizi hilo lilililenga daraja la Irfan mjini humo. Kwingineko jeshi la Yemen kwa kushirikiana na harakati ya wananchi ya Answarullah imeangamiza askari vibaraka wa Saudia waliokuwa wanakimbia uwanja wa mapigano baada ya kuzidiwa. Kwa mujibu wa habari hiyo askari kadhaa vibaraka wa Aal-Saud wameangamizwa katika mkoa wa Taiz kusini magharibi mwa Yemen.

Sehemu ya jinai za utawala wa kidikteta wa Aal-Saud huko Yemen

Hii ni katika hali ambayo kwa mara nyingine jeshi la Yemen limezilenga kambi za jeshi la Saudia za Jizan na kuisababisha nchi hiyo kibaraka wa Marekani na Israel hasara ya maafa na uharibifu. Kama ambavyo jeshi hilo la Yemen na harakati ya Answarullah limeshambulia kwa makombora mengi kambi ya jeshi ya al-Makhruq iliyopo eneo la Quwah mkoani Najran na kuangamiza askari kadhaa.