Wanajeshi wa Saudia waendeleza hujuma katika mji wa Al Awamiyah
https://parstoday.ir/sw/news/west_asia-i29558-wanajeshi_wa_saudia_waendeleza_hujuma_katika_mji_wa_al_awamiyah
Baada ya kupita wiki mbili tokea wanajeshi wa Saudi Arabia wavamie mtaa wa Al Masourah mjini Al-Awamiya mashariki mwa nchi hiyo hali inaripotiwa kuwa mbaya huku ukandamizaji ukiendelea.
(last modified 2026-01-14T08:12:18+00:00 )
May 24, 2017 23:56 UTC
  • Wanajeshi wa Saudia waendeleza hujuma katika mji wa Al Awamiyah

Baada ya kupita wiki mbili tokea wanajeshi wa Saudi Arabia wavamie mtaa wa Al Masourah mjini Al-Awamiya mashariki mwa nchi hiyo hali inaripotiwa kuwa mbaya huku ukandamizaji ukiendelea.

Wanajeshi wa Saudia wameteketeza moto misikiti, nyumba za raia na shule katika mtaa huo huku jamii ya kimataifa ikiwa inaendelea kunyamazia kimya jinai hiyo.

Siku ya Jumatano wanajeshi wa Saudia waliendeleza hujuma mashariki mwa Saudia kwa kudondosha mabomu katika eneo hilo.

Mabuldoza na magari ya deraya ya utawala wa Saudia katika kijiji cha al Masourah

Watawala wa Saudia wanataka kukiharibu kijiji cha al-Masourah ambako ndiko alikozaliwa Sheikh Nimri Baqir an-Nimr, mwanazuoni mkubwa wa Waislamu wa Kishia aliyeuawa kwa kukatwa kichwa na utawala huo mwaka jana. Watawala hao wa Saudia wamekivamia kijiji hicho kwa madai ya eti kukiboresha.

Kijiji cha al-Masourah kinafahamika kama nembo ya malalamiko huko mashariki mwa Saudia dhidi ya watawala wa nchi hiyo ya kidikteta.