-
Albanese: Misri inaunga mkono mauaji ya halaiki ya Wapalestina
Dec 22, 2025 02:51Ripota Maalum wa Umoja wa Mataifa ameitaja hatua ya Misri ya kuidhinisha makubaliano ya ununuzi wa gesi kutoka kwa utawala wa Israel kuwa ni uungaji mkono wa nchi hiyo kwa mauaji ya halaiki yanayofanywa na Wazayuni huko Gaza.
-
Hali mbaya ya wakimbizi Wazayuni; ukurasa wa kuuza viporo wapata umaarufu Israel
Dec 22, 2025 02:50Ukurasa mmoja wa mitandao ya kijamii unaouza viporo na masalia ya chakula yaliyobaki mikahawani umepata umaarufu mkubwa huko Israel kiasi kwamba kutokana na hali ngumu ya maisha, Wazayuni wengi wanajitokeza kwenye ukurasa huo kununua chakula kilichobaki mikahawani na matunda yaliyoharibika madukani.
-
Maulamaa wa Yemen walaani kuvunjiwa heshima Qur'ani Tukufu nchini Marekani
Dec 21, 2025 12:16Maulamaa na wanazuoni wa Yemen wamelaani kuvunjiwa heshima Qur'ani Tukufu nchini Marekani. Tukio la hivi karibuni la uhalifu huo limefanywa na mgombea mmoja wa Baraza la Seneti la Marekani.
-
Israel yaendelea kumwaga damu za Wapalestina Gaza, Ukingo wa Magharibi
Dec 21, 2025 11:13Wapalestina wawili, akiwemo kijana mmoja, wameuawa shahidi huku wengine wawili wakijeruhiwa kwa risasi baada ya vikosi vya Israel kufanya mashambulizi tofauti katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan, katika ghasia za hivi punde dhidi ya Wapalestina wa eneo hilo linalokaliwa kwa mabavu.
-
Kwa nini mpango wa Al‑Ahram kuhusu usalama wa Asia Magharibi ni wa kupotosha na ni hatari?
Dec 21, 2025 07:57Tovuti ya Ahram Online (sehemu ya Kiingereza ya gazeti la Al-Ahram la Misri) katika makala yake imependekeza kufanyika kwa mkutano wa usalama katika eneo la Asia ya Magharibi, kwa ushiriki wa madola yenye nguvu zaidi duniani, ili kuzuia kuanza tena kwa vita kati ya Iran na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Picha za satelaiti zaonyesha Israel ikijimarisha kuwepo kijeshi katika Ukanda Gaza
Dec 21, 2025 07:56Utawala wa Israel unaonekana kuandaa mazingira ya kudumisha uwepo wake kijeshi katika maeneo makubwa ya Ukanda wa Gaza. Hii ni kwa mujibu wa uchambuzi mpya wa picha za satelaiti ulioweka wazi ujenzi mkubwa, upanuzi wa miundombinu na kuendelea kuharibiwa mali za Wapalestina tangu kutekelezwa mapatano ya usitishaji vita mwezi Oktoba.
-
Ripoti: Watoto wa Gaza wanateseka na baridi kali
Dec 21, 2025 02:35Dhoruba za majira ya baridi kali zimesababisha vifo vya Wapalestina wasiopungua 17 katika Ukanda wa Gaza mwezi huu wa Disemba pekee.
-
Hamas yalaani shambulizi la kikatili dhidi ya shule katika mji wa Gaza
Dec 20, 2025 12:54Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imelaani shamulizi la kikatili la Israel dhidi ya shule moja katika mji wa Gaza lililouwa Wapalestina kadhaa. Hamas imeitaja hujuma hiyo kuwa jinai ya kivita ya makusudi na ukiukaji wa wazi wa mapatano ya kusitisha mapigano.
-
Katibu Mkuu wa UN akemea kuongezeka kwa ukatili wa walowezi wa Kizayuni Ukingo wa Magharibi
Dec 20, 2025 07:06Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, amelaani kuongezeka kwa mashambulizi ya walowezi wa Kizayuni wasiokuwa halali dhidi ya raia wa Kipalestina wasio na silaha na mali zao katika maeneo ya Ukingo wa Magharibi yanayokaliwa kwa mabavu na Israel.
-
Wayemen waandamana kupinga kuvunjiwa heshima Qur'an Marekani
Dec 20, 2025 02:38Makumi ya maelfu ya wananchi wa Yemen walimiminika katika barabara na mitaa ya Sa’ada jana Ijumaa kushiriki maandamano ya kulaani kitendo cha kunajisiwa Qur'ani Tukufu nchini Marekani, sanjari na kupaza sauti zao kuiunga mkono Palestina, huku hasira zikiongezeka katika ulimwengu wa Kiislamu kutokana na wimbi la vitendo vya hivi karibuni vilivyo dhidi ya Uislamu na Waislamu.