-
Rais wa Pakistan: Israel lazima iwajibike kwa uhalifu wa kivita Gaza
Nov 30, 2025 07:39Rais wa Pakistan Asif Ali Zardari ametoa pongezi kwa wananchi wa Palestina katika maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Mshikamano na Palestina akisema: "Juhudi na ujasiri wenu usio wa kuchoka umeunda sura mpya katika historia."
-
Foleni za watu wenye njaa huko Ghaza zimezidi kuwa ndefu + Picha
Nov 30, 2025 02:36Licha ya kusitishwa mapigano huko Ghaza, lakini bado mateso ya njaa na ukosefu wa usalama na utulivu wa nafsi yanaendelea kuzisumbua familia za Wapalestina. Foleni ndefu za watu wenye njaa wanaosubiri kupata angalau mlo mmoja kwa siku zinaendelea kuonekana katika pembe mbalimbali za ukanda huo huku jeshi katili la Israeli likiendeleza mashambulizi ya mara kwa mara na kuzuia kuwafikia misaada wananchi hao wasio na ulinzi.
-
Israel: Hatuna mpango kabisa wa kuondoka kusini mwa Syria
Nov 30, 2025 02:35Jeshi la Israel limejigamba kuwa halina mpango kabisa wa kuondoka kwenye ardhi ulizozivamia na kuzikalia kwa mabavu huko Syria licha ya wanajeshi wake sita kujeruhiwa wakati wananchi wa Syria walipoamua kupambana na Wazayuni hao maghasibu.
-
Hizbullah: Tutaamua 'wakati na mahala' pa kutolea jibu la mauaji ya Tabatabai yaliyofanywa na Israel
Nov 29, 2025 11:15Katibu Mkuu wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya nchini Lebanon ya Hizbullah amesema, harakati hiyo ina haki ya kutoa jibu kwa shambulio la kigaidi lililofanywa na utawala wa kizayuni wa Israel lililomuua Kamanda wake mwandamizi Haytham Ali Tabatabai, na akaongeza kuwa Hizbullah yenyewe itaamua wakati na mahali pa kutolea jibu hilo.
-
Amnesty International: Israel inaendelea kufanya mauaji ya kimbari Ghaza
Nov 29, 2025 11:14Shirika la kimataifa la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limetangaza kuwa, utawala wa kizayuni wa Israel "unaendelea bila kusita kufanya mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina huko Ghaza, licha ya usitishaji mapigano" ulioanza kutekelezwa tarehe 10 Oktoba.
-
Kwa nini Mamlaka ya Ndani ya Palestina imezidi kuwatia nguvuni watu kwa malengo ya kisiasa?
Nov 29, 2025 09:22Hatua ya Mamlaka ya Ndani ya Palestina ya kuzidisha kasi ya kuwatia mbaroni watu kwa malengo ya kisiasa katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan imekabiliwa na upinzani na wasiwasi wa Wapalestina kuhusiana na matokeo mabaya ya hatua hiyo.
-
Uvamizi wa kijeshi wa Israel nchini Syria walaaniwa na Iran na nchi za Kiarabu
Nov 29, 2025 07:15Uvamizi wa nchi kavu na anga uliofanywa na jeshi la Israel katika mji wa Beit Jinn, kusini mwa Syria, ambapo watu wasiopungua 13, wakiwemo watoto, waliuawa umelaaniwa vikali na Iran pamoja na mataifa kadhaa ya Ghuba ya Uajemi.
-
Sana’a yalaani uingiliaji wa Marekani katika masuala ya Yemen
Nov 28, 2025 11:42Serikali ya Yemen imelaani vikali hatua ya Marekani ya kuingilia masuala ya ndani ya nchi hiyo ya Kiarabu na kuitaja kuwa isiyokubalika.
-
Israel yatumia mfumo wa akili mnemba (AI) kufuatilia mitandao ya kijamii ya wanajeshi, ili kuzuia ushahidi wa uhalifu wa kivita
Nov 28, 2025 02:59Jeshi la Israel limezindua mradi mkubwa wa akili mnemba (AI), unaojulikana kama Morpheus, ili kuzuia askari wake kuchapisha ushahidi wa uhalifu wa kivita uliofanyika huko Gaza kwenye mitandao ya kijamii.
-
Hamas yakemea mauaji na mateso ya wafungwa Wapalestina magerezani Israel
Nov 27, 2025 12:19Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestima (Hamas) imelaani vikali mauaji ya makusudi na mateso ya Wapalestina walioko katika magereza ya kuogofya ya utawala haramu wa Israel, ikiyataja kama “uhalifu kamili wa kivita” na kuitaka jamii ya kimataifa kuchukua hatua madhubuti dhidi ya uhalifu huo.