Ynetnews: Trump amemuahidi Netanyanu atamruhusu akiuke makubaliano mapya ya Ghaza
Rais mteule wa Marekani Donald Trump ameahidi kumruhusu waziri mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel Benjamin Netanyahu aanze tena kufanya mauaji ya kimbari katika Ukanda wa Ghaza baada ya kutia saini makubaliano yanayotarajiwa kutangazwa wakati wowote kutoka sasa ya kusitisha mapigano na harakati ya Hamas. Hayo yameelezwa na duru za habari za Israel.
Hata hivyo mashinikizo ya umma na ya kidiplomasia dhidi ya utawala wake yamekuwa yakiongezeka kuutaka ufikie makubaliano ya kusitisha vita ili kuachiwa huru mateka wa Kizayuni wanaoshikiliwa Ghaza na mahabusu wa Kipalestina wanaoteseka kwenye magereza ya utawala huo wa Kizayuni.
Kwa upande wao, makundi ya Muqawama wa Wapalestina yameonyesha muda wote kuwa na nia ya kufikia makubaliano ya kusimamisha vita ili kuhitimisha mateso makubwa wanayohimili Wapalestina wa Ukanda wa Ghaza.../