Mashindano ya Kimataifa ya Qurani yamalizika Moscow, Russia
https://parstoday.ir/sw/news/world-i90798-mashindano_ya_kimataifa_ya_qurani_yamalizika_moscow_russia
Duru ya 20 ya Mashindano ya Kimataifa ya Qurani Tukufu iliyoanza Ijumaa iliyopita katika mji mkuu wa Russia, Moscow imemalizika huku washindi wakitangazwa na kutuzwa.
(last modified 2023-11-27T08:44:11+00:00 )
Nov 21, 2022 07:45 UTC
  • Mashindano ya Kimataifa ya Qurani yamalizika Moscow, Russia

Duru ya 20 ya Mashindano ya Kimataifa ya Qurani Tukufu iliyoanza Ijumaa iliyopita katika mji mkuu wa Russia, Moscow imemalizika huku washindi wakitangazwa na kutuzwa.

Raia wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Sayyid Mostafa Hosseini ameibuka mshindi wa tatu kwenye mashindano hayo ya dunia yaliyofanyika katika Msitiki wa Jamia jijini Moscow.

Nafasi ya kwanza imetwaliwa na msomaji wa Qurani Tukufu kutoka Uturuki, akifuatiwa na qarii mwingine wa Kitabu Kitukufu cha Waislamu raia wa Misri.

Wasomaji wengine wa walioshiriki mashindano hayo wametoka katika nchi za Kuwait, Iraq, Tajikistan, Uzbekistan, Lebanon, Imarati, Sudan, Misri, Morocco, Kazakhstan, Syria, Bangladesh, na Yemen.

Kanda ya Afrika Mashariki imewakilishwa na Tanzania kwenye mashindano hayo ya kimataifa ya kusoma Qurani kwa kuzingatia kanuni za tajwidi.

Msikiti Mkubwa wa Jamaa Moscow 

Mashindano hayo ya Kimataifa ya Qurani Tukufu yameandaliwa na Baraza la Mamufti la Russia kwa ushirikiano na Jumuiya ya Waislamu Duniani.

Hii ni mara ya kwanza kwa mashindano hayo kuandaliwa baada ya kusitishwa kwa miaka miwili, kutokana na janga la Corona lililosimamisha shughuli nyingi za kiuchumi na kijamii duniani.