-
Mkuu wa Majeshi Algeria: Uchaguzi ni njia bora ya kujinasua na mgogoro
May 21, 2019 04:45Mkuu wa Majeshi wa Algeria alisema jana Jumatatu katika taarifa aliyotoa kupitia televisheni ya nchi hiyo kuwa kufanyika uchaguzi ni njia bora itakayoiwezesha Algeria kuondoka na mgogoro wa kisiasa na kuepuka ombwe la kikatiba.
-
Algeria yawakamata wahamiaji haramu 95
May 14, 2019 04:16Vikosi vya usalama Algeria vimewakamata wahamiaji haramu 95 kwenye operesheni mbalimbali.
-
Uchaguzi; changamoto kubwa katika matukio ya Algeria
May 08, 2019 01:26Mgogoro wa kisiasa nchini Algeria unaendelea kushuhudiwa huku suala la kufanyika uchaguzi wa Rais limegeuka na kuwa changamoto kubwa kabisa nchini humo.
-
Rais wa muda wa Algeria ataka kuweko mazungumzo ya kitaifa
May 07, 2019 04:11Abdelkader Bensalah, Rais wa Muda wa Algeria ametoa wito wa kuweko mazungumzo ya kitaifa katika nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika kwa shabaha ya kufikia mwafaka katika masuala ambayo yamezusha hitilafu nchini humo.
-
Maandamano ya wananchi yaendelea Algeria kupinga serikali ya mpito
May 04, 2019 08:13Wananchi wa Algeria wameendelea na maandamano yao ya kupinga serikali ya mpito ya nchi hiyo na kuishutumu kuwa inapoteza muda.
-
Waandamanaji Algeria wataka kupandishwa kizimbani ndugu ya Bouteflika
Apr 27, 2019 02:41Wananchi wa Algeria jana waliandamana tena ikiwa ni Ijumaa ya 10 mtawalia ya maandamano yao ambapo mbali na kusisitiza juu ya kuachia ngazi viongozi na maafisa wote wa serikali waliokuwa katika kipindi cha utawala wa Abdelaziz Bouteflika, Rais wa nchi hiyo aliyelazimika kujiuzulu, wametoa mwito wa kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria Said Bouteflika, ndugu ya rais huyo mkongwe aliyejiuzulu kufuatia maandamano ya wananchi.
-
Mwenyekiti wa Baraza la Katiba Algeria ajiuzulu huku maandamano yakiendelea
Apr 17, 2019 02:26Mwenyekiti wa Baraza la Katiba nchini Algeria amejiuzulu huku maandamano ya wananchi yakiendelea katika miji mbalimbali ya nchi hiyo.
-
Majaji wa Algeria kususia uchaguzi mkuu ujao wa Julai
Apr 14, 2019 07:44Majaji wa Algeria wametangaza kuwa watasusia uchaguzi mkuu ujao ulioratibiwa kufanyika mwezi Julai mwaka huu.
-
Uchaguzi wa rais wa Algeria kufanyika tarehe 4 Julai
Apr 11, 2019 03:15Ofisi ya rais wa Algeria imetangaza kuwa, uchaguzi wa rais wa nchi hiyo utafanyika tarehe 4 Julai mwaka huu.
-
Maandamano yanaendelea Algeria licha ya ahadi za kufanyika uchaguzi huru
Apr 10, 2019 16:10Polisi katika mji mkuu wa Algeria, Algiers wamewafyatulia mabomu ya kutoa machozi maelfu ya wanafunzi waliokuwa wanaandamana kumpinga Spika wa Bunge Abdelkader Bensalah anayekaimu nafasi ya Abdulaziz Bouteflika, rais wa Algeria aliyelazimishwa kujiuzulu na maandamano makubwa ya wananchi.