-
Ethiopia yamteua mwanamke mpinzani kuongoza Tume ya Uchaguzi
Nov 22, 2018 11:27Bunge la Ethiopia limemuidhinisha kiongozi mashuhuri wa upinzani aliyekuwa akiishi uhamishoni, Birtukan Mideksa kuwa mkuu mpya wa Tume ya Uchaguzi nchini humo.
-
Baraza la Usalama la UN laifutia vikwazo Eritrea
Nov 15, 2018 00:04Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeifutia vikwazo Eritrea kufuatia kusainiwa makubaliano ya amani ya kihistoria kati ya nchi hiyo na Ethiopia na kuboreka uhusiano baina yake na Djibouti pia.
-
Kaburi la umati lagunduliwa Ethiopia
Nov 09, 2018 04:21Serikali ya Ethiopia imetangaza kugunduliwa kaburi la umati lenye miili 200 katika eneo lililo baina ya maeneo ya Oromia na Somali yanayokumbwa na machafuko.
-
Homa ya Manjano yaua watu 10 nchini Ethiopia
Nov 06, 2018 04:33Shirika la Afya Duniani WHO limetangaza kuwa watu 10 wamepoteza maisha kutokana na Homa ya Manjano kusini magharibi Ethiopia.
-
Baraza la Usalama la UN kuiondolea vikwazo Eritrea
Nov 04, 2018 04:34Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa linatazamiwa kuiondolea vikwazo Eritrea ndani ya siku chache zijazo, ilivyowekewa mwaka 2009 kwa tuhuma za kuliunga mkono kundi la kigaidi na kitakfiri la al-Shabaab la nchi jirani ya Somalia.
-
Ethiopia yaondoa rasmi viza kwa Waafrika
Oct 27, 2018 04:04Waziri Mkuu wa Ethiopia, Abiy Ahmed jana alitangaza kuwa, kuanzia tarehe 9 mwezi ujao wa Novemba, nchi yake itawaondolea viza raia wote wa nchi za Afrika.
-
Ethiopia yapata rais wa kwanza mwanamke
Oct 25, 2018 10:25Bunge la Ethiopia limemuidhinisha mwandiplomasia wa kimataifa, Sahle-Work Zewde kuwa rais wa kwanza mwanamke wa nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.
-
Ethiopia yasaini makubaliano ya amani na kundi la waasi wa Ogaden
Oct 22, 2018 23:32Ethiopia imesema kuwa imesaini makubaliano ya amani na kundi lililokuwa likipigania kujitenga la Waasi wa Harakati ya Taifa ya Ukombozi wa Ogaden (ONLF) na hivyo kuhitimisha rasmi uasi uliodumu kwa zaidi ya miongo mitatu katika mkoa wa Somalia mashariki mwa nchi hiyo.
-
Ethiopia yawaachia huru watu 1,174 waliohusishwa na machafuko ya Addis Ababa
Oct 18, 2018 12:54Serikali ya Ethiopia imetangaza habari ya kuachiwa huru mamia ya watu waliokamatwa wakati wa ghasia zilizoshuhudiwa mwezi uliopita wa Septemba katika mji mkuu, Addis Ababa.
-
Kwa mara ya kwanza, Mwislamu mwanamke ateuliwa kuwa Waziri wa Ulinzi Ethiopia
Oct 17, 2018 05:25Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed Ali amemteua mwanamke Mwislamu kuwa Waziri wa Ulinzi wa nchi hiyo, hii ikiwa ni mara ya kwanza kabisa katika historia ya nchi hiyo.