-
Morocco yaelekea Afrika Mashariki kutafuta uungaji mkono AU
Oct 20, 2016 10:04Mfalme Mohammed wa VI wa Morocco ameanza ziara ya nchi tatu za Afrika Mashariki katika juhudi za kutafuta uungaji mkono wa kurejea nchi hiyo kuwa mwananchama wa Umoja wa Afrika, baada ya kujiondoa kwenye umoja huo zaidi ya miongo mitatu iliyopita.
-
UN: Hali ya hatari Ethiopia inalenga wanadiplomasia na wanahabari
Oct 18, 2016 03:34Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-moon, amesema anafuatilia kwa karibu matukio ya hivi sasa nchini Ethiopia na kueleza wasi wasi wake kuwa hali ya hatari iliyotangazwa hivi karibuni na serikali ya Addis Ababa, inawaathiri zaidi wanadiplomasia na waandishi wa habari.
-
Ethiopia yapitisha sheria kali zaidi za hali ya hatari
Oct 17, 2016 10:49Wizara ya Ulinzi ya Ethiopia imetangaza habari ya kuanzisha sheria kali zaidi za hali ya hatari nchini humo.
-
Waziri Mkuu wa Ethiopia ataka kusitishwa haraka machafuko
Oct 10, 2016 10:14Waziri Mkuu wa Ethiopia ametaka kusiitishwa haraka iwezekanavyo ghasia za kisiasa nchini humo.
-
Kuendelea malalamiko na maandamano ya wananchi nchini Ethiopia
Oct 08, 2016 09:16Malalamiko ya wananchi na maandamano ya wapinzani wa kisiasa wa serikali ya sasa ya Ethiopia yangali yanaendelea.
-
Waandamanaji wenye hasira washambulia viwanda vya makampuni ya kigeni nchini Ethiopia
Oct 08, 2016 00:34Wananchi wenye hasira wamebomoa na kuharibu makumi ya viwanda vinavyomilikiwa na makampuni ya kigeni, mashamba ya maua pamoja na kuchoma moto magari kadhaa kulalamikia kile wanachoeleza uporaji ardhi zao unaofanywa na serikali nchini Ethiopia.
-
Viongozi wawili wa upinzani nchini Ethiopia watiwa nguvuni
Sep 12, 2016 23:45Duru za kuaminika zimeripoti kuwa viongozi wawili wa upinzani nchini Ethiopia wametiwa nguvuni.
-
Ethiopia yaachilia huru mamia ya wafungwa wakiwemo Waislamu
Sep 12, 2016 03:34Ethiopia imetangaza kuwaachilia huru mamia ya wafungwa wakiwemo Waislamu ambao walikuwa wanashikiliwa kwa kupinga uingiliaji wa serikali katika mambo yao ya kidini.