-
Raisi: Msingi wa uhusiano wa Iran na Afrika ni maslahi ya pamoja
Jan 25, 2024 07:43Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema uhusiano wa Iran na Mali pamoja na nchi nyingine za Afrika si wa kisiasa na kidiplomasia tu, bali umejengeka katika msingi wa maslahi ya pande mbili na pande kadhaa.
-
Marais wa Iran na Uturuki wasaini hati 10 za ushirikiano
Jan 25, 2024 03:36Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Uturuki zimetia saini hati 10 za ushirikiano kwa lengo la kuzidisha uwekezaji, ushirikiano wa kiuchumi na masuala ya kieneo.
-
Wairani wajitokeza kwa wingi kuwaaga mashahidi wa shambulizi la kigaidi la Israel
Jan 22, 2024 08:38Shughuli ya kuwaaga mashahidi wa shambulizi la kigaidi la Israel nchini Syria imefanyika hapa Tehran kwa kuhudhuriwa na viongozi wa ngazi ya juu, familia za mashahidi hao na umati mkubwa wa wananchi Waislamu wa Iran.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran kuitembelea Misri karibuni
Jan 22, 2024 08:35Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Hossein Amir-Abdollahian anataziwa kuitembelea Misri ndani ya siku chache zijazo, huku utawala wa Kizayuni ukiingiwa na kiwewe kutokana na kuendelea kuimarika uhusiano wa Tehran na Cairo.
-
Raisi: Iran inaunga mkono kesi ya Afrika Kusini dhidi ya Israel ICJ
Jan 22, 2024 04:01Rais wa Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu inaunga mkono uamuzi wa 'busara' na wa 'kihistoria' wa Afrika Kusini wa kuwasilisha kesi dhidi ya utawala haramu wa Israel katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ), kuhusu jinai za mauaji ya kimbari zinazotekelezwa na utawala huo dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza.
-
Kan'ani: Kuna uhusiano mkubwa kati ya utawala gaidi wa Israel na Daesh
Jan 21, 2024 04:22Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amelaani vikali jinai na uchokozi uliofanywa mapema jana na utawala wa Kizayuni wa Israel katika eneo la raia huko al Mezza, Damascus mji mkuu wa Syria na kuuwa shahidi washauri watano wa kijeshi wa Iran na askari kadhaa wa Syria.
-
Pakistan yatangaza kurejesha uhusiano kamili na Iran baada ya mivutano iliyojitokeza
Jan 20, 2024 03:23Pakistan imetangaza kurejesha kikamilifu uhusiano wa kidiplomasia na Iran baada ya kujitokeza mivutano mikali ya mpakani ambayo haijawahi kushuhudiwa kati ya nchi mbili juu ya operesheni za kupambana na ugaidi.
-
Magaidi kadhaa wa shambulio la Kerman wauawa, baadhi wakamatwa
Jan 20, 2024 00:33Wizara ya Usalama wa Taifa ya Iran imesema vikosi vyake vimefanikiwa kuwaangamiza na kuwatia mbaroni magaidi kadhaa wa shambulio la kigaidi la mapema mwezi huu katika mji wa Kerman, kusini mashariki mwa Iran lililopelekea kuuawa shahidi na kujeruhiwa makumi ya watu.
-
Iran yakosoa taarifa ya Arab League, yasema itaendelea kuwaadhibu watenda jinai
Jan 19, 2024 08:16Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amekosoa vikali taarifa ya Jumuiya ya Nchi za Kiarabu kuhusu hatua ya Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) ya kufanya shambulio la makombora dhidi ya kituo kikuu cha ujasusi cha shirika la ujasusi la utawala wa Kizayuni wa Israel Mossad katika eneo la Kurdistan ya Iraq.
-
Iran yaikosoa US kwa kuiweka Ansarullah katika orodha ya 'ugaidi'
Jan 19, 2024 00:00Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amelaani vikali hatua ya Marekani ya kuiweka Harakati ya Ansarullah ya Yemen kwenye orodha ya kile inachokiita "makundi ya kigaidi" na kueleza kwamba, kitendo hicho ni katika mfululizo wa hatua za Washington za kuuunga mkono utawala wa kigaidi wa Israel.