-
Iran: Mashambulizi ya Israel dhidi ya Aleppo yanakiuka sheria za kimataifa
Mar 23, 2023 23:18Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa amelaani mashambulizi ya anga ya hivi karibuni ya utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa Aleppo (Halab) huko kaskazini mwa Syria na kusisitiza kuwa, uvamizi huo unakanyaga sheria za kimataifa, Hati ya Umoja wa Mataifa mbali na kuwa tishio kubwa kwa amani na uthabiti wa eneo la Asia Magharibi.
-
Raisi awapongeza viongozi wa nchi za Kiislamu kwa kuanza Ramadhani
Mar 23, 2023 07:48Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amewatumia salamu za pongezi viongozi wa nchi za Kiislamu kwa kuanza mwezi mtukufu wa Ramadhani.
-
GCC: Mapatano ya Saudia, Iran kuhitimisha migogoro katika eneo
Mar 23, 2023 07:41Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi (GCC) limepongeza makubaliano ya hivi karibuni kati ya Iran na Saudi Arabia ya kurejesha uhusiano wa kidiplomasia uliokuwa umevunjika kwa kipindi cha miaka saba.
-
Mapatano ya Kiusalama kati ya Iran na Iraq; azma thabiti ya kukabiliana na vitisho
Mar 22, 2023 22:43Katika hafla iliyohudhuriwa na Mohammad Shia as-Sudani, Waziri Mkuu wa Iraq hapo siku ya Jumapili tarehe 19 Machi mwaka huu, makubaliano ya ushirikiano wa usalama wa pamoja wa kati ya nchi mbili jirani za Iran na Iraq yalitiwa saini na Admeri Ali Shamkhani, Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Kitaifa la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, na Qasim al-Aarji, Mshauri wa Usalama wa Kitaifa wa Waziri Mkuu wa Iraq.
-
Mapatano ya Kiusalama kati ya Iran na Iraq; azma thabiti ya kukabiliana na vitisho
Mar 21, 2023 22:47Katika hafla iliyohudhuriwa na Mohammad Shia as-Sudani, Waziri Mkuu wa Iraq hapo siku ya Jumapili tarehe 19 Machi mwaka huu, makubaliano ya ushirikiano wa usalama wa pamoja wa kati ya nchi mbili jirani za Iran na Iraq yalitiwa saini na Admeri Ali Shamkhani, Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Kitaifa la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, na Qasim al-Aarji, Mshauri wa Usalama wa Kitaifa wa Waziri Mkuu wa Iraq.
-
Mawaziri wa Mambo ya Nje wa OIC wapongeza mapatano ya Iran na Saudia
Mar 18, 2023 04:36Mawaziri wa Mambo ya Nje wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) wamepongeza makubaliano ya hivi karibuni kati ya Iran na Saudi Arabia ya kurejesha uhusiano wa kidiplomasia.
-
Mufti wa Oman: Mapatano ya Iran na Saudia yameutia hofu na kiwewe utawala wa Kizayuni wa Israel
Mar 18, 2023 00:37Mufti wa Oman Sheikh Ahmad bin Hamad Al-Khalili amesisitiza haja ya kudumishwa amani na utangamano katika eneo la Ghuba ya Uajemi na kubainisha kwamba, makubaliano na mapatano yaliyofikiwa kati ya Iran na Saudi Arabia yameutia hofu na kiwewe utawala haramu wa Kizayuni wa Israel.
-
Mazoezi ya pamoja ya majeshi ya majini ya Iran, China na Russia
Mar 16, 2023 22:45Mazoezi ya pamoja ya majeshi ya majini ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, China na Russia yanayofanyika kwa anwani ya "Ukanda wa Amani wa Baharini 2023", yameakisiwa sana kimataifa na kuwa habari ya kwanza katika vyombo mashuhuri vya habari duniani.
-
Msimamo wa Iran kwa mnasaba wa Machi 15, Siku ya Kimataifa ya Kupambana na Chuki dhidi ya Uislamu
Mar 16, 2023 08:17Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran jana Jumatano alituma ujumbe katika ukurasa wake wa Twitter akisema kwamba: Wale wenye chuki dhidi ya Uislamu na Waislamu hawaamini maadili yoyote ya kibinadamu na dini za Mwenyezi Mungu.
-
Iran, China na Russia zafanya luteka ya pamoja katika Bahari ya Oman
Mar 16, 2023 07:55Vikosi vya majini vya Iran, Russia na China vinaendelea na mazoezi ya pamoja ya kijeshi katika Bahari ya Oman, huo ukiwa ni muendelezo wa juhudi za nchi tatu hizo za kuimarisha ushirikiano wa majeshi yao ya baharini.