-
Bunge la Iran lapinga kuondolewa vikwazo taifa hili hatua kwa hatua
Apr 04, 2021 07:31Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) imepinga pendekezo la kuondolewa vikwazo taifa hili hatua kwa hatua.
-
Iran yalaani kufunguliwa ubalozi wa Bahrain mjini Tel Aviv
Apr 04, 2021 03:25Kongamano la Kimataifa la Kuunga Mkono Intifadha ya Palestina katika Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu, Bunge la Iran, limelaani hatua ya utawala wa kifalme wa Bahrain kufungua ubalozi katika utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Kamati ya pamoja ya Iran na Iraq yachunguza mauaji ya kigaidi ya Soleimani
Apr 03, 2021 05:13Mkuu wa Baraza Kuu la Haki za Binadamu la Vyombo vya Mahakama vya Iran amesema faili la mauaji ya kigaidi ya Shahid Qassem Soleimani, aliyekuwa Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la Iran (IRGC) linafuatiliwa na kamati ya pamoja ya Iran na Iraq.
-
Iran yaipa Kenya msaada wa vifaa vya kupambana na Corona
Apr 02, 2021 22:16Kenya imepokea msaada wa suhula za matibabu na vifaa vya kukabiliana na ugonjwa wa Covid-19 kutoka Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Zarif: Hakuna udharura wa kufanyika mkutano kati ya Iran na Marekani
Apr 02, 2021 22:10Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema hakuna mazungumzo yoyote yatakayofanyika baina ya Jamhuri ya Kiislamu na Marekani juu ya kuhuisha makubaliano ya nyuklia ya JCPOA, na kwamba hakuna udharura wa kufanyika mkutano baina Tehran na Washington.
-
Rouhani: Ni zamu ya kundi la 5+1 kutekeleza wajibu wake mkabala wa Iran
Apr 01, 2021 07:10Rais Hassan Rouhani wa Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu imetekeleza barabara wajibu wake na kufungamana na ahadi zake katika makubaliano ya nyuklia ya JCPOA, na hivi sasa ni zamu ya kundi la 5+1 kutekeleza jukumu lake.
-
Naim Qassim: Kushikamana Waislamu kumesambaratisha njama za US-Israel
Apr 01, 2021 06:05Naibu Katibu Mkuu wa harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesema kuungana na kushikamana Waislamu pasina kujali tofauti zao za kimitazamo na kiitikadi kumesambaratisha njama za Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel za kuyagawanya vipande vipande mataifa ya Kiislamu.
-
Rais Rouhani: Endapo Marekani itatekeleza ahadi zake, sisi pia tutafanya hivyo
Mar 31, 2021 07:20Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, endapo kutakuwa na azma imara na Marekani ikarejea katika mazingira ya kabla ya vikwazo, sisi pia siku hiyo hiyo tutaanza kutekeleza ahadi zetu.
-
White House: Tunachunguza uwezekano wa kutekeleza vikwazo baada ya mapatano yaliyofikiwa kati ya Iran na China
Mar 30, 2021 03:25Msemaji wa White House ametoa radiamali yake kufuatia kusainiwa mpango wa ushirikiano wa kimkakati wa miaka 25 kati ya Iran na China.
-
Ali Shamkhani: Ushirikiano wa kistratejia Mashariki unaharakisha kusambaratika Marekani
Mar 29, 2021 03:45Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran amesema kuwa, ushirikiano wa kistratejia wa Mashariki utaharakisha kusambaratika Marekani.