-
Grossi apongeza mapatano yaliyofikiwa kati ya wakala wa IAEA na Iran
Sep 21, 2020 23:05Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Nyuklia (IAEA) kwa mara nyingine tena amepongeza mapatano yaliyofikiwa baina ya wakala huo na Jamhuri ya Kiislamu Iran.
-
Mazoezi ya kijeshi ya Kavkaz-2020 yaanza leo nchini Russia, Iran na China zinashiriki
Sep 21, 2020 10:07Mazoezi ya pamoja ya kijeshi yaliyopewa jina la Kavkaz-2020 yamenza leo yakishirikisha wanajeshi elfu 13 kutoka nchi za Iran, China, Pakistan, Belarus, Myanmar na mwenyeji Russia katika eneo la kusini mwa nchi hiyo.
-
Msimamo mmoja wa kundi la 4+1 mbele ya madai hewa ya Marekani kuhusu Iran
Sep 21, 2020 07:03Licha ya Marekani kutoa madai hewa ya kuanza kutekelezwa vikwazo vya kimataifa dhidi ya Iran kuanzia jana Jumapili Septemba 20, 2020 vikiwemo vikwazo vya silaha, lakini mataifa ya dunia yamepinga madai hayo ya Washington na yamechukua msimamo imara kiasi kwamba inaonekana kama vile hakuna mabadiliko yoyote yaliyotokea.
-
Khatibazadeh: Marekani inajua madai yake ya vikwazo dhidi ya Iran ni hewa
Sep 20, 2020 22:56Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya Iran amesema tangazo la Marekani kwamba vikwazo vyote vya Umoja wa Mataifa dhidi ya Tehran ambavyo vilikuwa vimeondolewa eti vimerejeshwa upya ni madai hewa, yasio na athari yoyote na yaliyo kinyume cha sheria.
-
Vurugu na machafuko Asia Magharibi; natija ya sera za Marekani
Sep 20, 2020 22:56Marekani kwa mara nyingine tena imetoa taarifa ikiituhumu Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwamba, eti inazusha vurugu na machafuko katika eneo la Asia Magharibi.
-
Madai ya Marekani kuhusu kurejeshwa vikwazo vya kimataifa dhidi ya Iran; ndoto na kujidanganya kwake
Sep 20, 2020 05:56Kugonga mwamba Marekani katika juhudi zake za kutaka muda wa vikwazo vya silaha dhidi ya Iran uongezwe katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, kuliifanya serikali ya Donald Trump sambamba na kuibuka na madai kuwa, ni mwanachama wa makubaliano ya nyuklia ya JCPOA na kwamba, Iran imekiuka makubaliano hayo, ilidai kurejea upya vikwazo vya kimataifa dhidi ya Tehran na ikatoa muhula wa mwezi mmoja katika uwanja huo
-
Vyombo vya Usalama Afrika Kusini: Hakuna ushahidi wa madai ya US dhidi ya Iran
Sep 19, 2020 08:26Idara ya Usalama wa Taifa ya Afrika Kusini imesema hakuna ushahidi wowote iliyoupata wa madai ya Marekani kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inapanga kumuua Lana Marks, Balozi wa Marekani katika nchi hiyo ya kusini mwa Afrika.
-
Afrika Kusini yakadhibisha tuhuma za Marekani dhidi ya Iran
Sep 19, 2020 06:34Baada ya Marekani kujiondoa katika makubaliano ya nyuklia ya JCPOA, serikali ya Rais Donald Trump ilizidisha mashinikizo ya kiwango cha juu dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa shabaha ya eti kulemaza uchumi wa Iran na imekuwa ikitumia kila liwezekanalo kuanzisha vita vya kinafsi na kisaikolojia ikiwa ni pamoja na kutoa vitisho dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu.
-
Tarehe 20 Septemba; Marekani kupata pigo jingine?
Sep 18, 2020 23:57Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, hakuna kitu kipya kitakachotokea kesho tarehe 20 Septemba na kwamba, inamtosha kwa Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Marekani kulisoma azimio nambari 2231 la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
-
Waziri Zarif amjibu Pompeo: Hakuna kitu kipya kitakachofanyika Septemba 20
Sep 18, 2020 03:39Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amejibu matamshi ya hivi karibuni ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Mike Pompeo juu ya njama za Washington za kutaka kurejesha vikwazo vya Umoja wa Mataifa dhidi ya Iran kwa kutumia mchakato unaofahamika kama 'Snapback Mechanism' na kusisitiza kuwa, 'Hakuna kitu maalumu kitakachofanyika Jumapili ya Septemba 20.'