Jan 26, 2024 07:57
Afisa mmoja wa Marekani ambaye hakutaka jina lake litajwe amesema, katika barua ambayo balozi wa Marekani mjini Baghdad, Alina Romanovsky aliiwasilisha siku ya Jumatano kwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Iraq Fuad Hossein, Washington imetangaza kuwa iko tayari kuanza mazungumzo na Baghdad ya kuhitimisha uwepo kijeshi wa nchi hiyo na washirika wake katika ardhi ya Iraq.