-
Iraq: Muungano wa kijeshi unaoongozwa na Marekani kuondoa wanajeshi wake huko Iraq katika muda wa miaka 2
Sep 09, 2024 10:48Iraq imesema kuwa muungano wa kijeshi unaoongozwa na Marekani, ambao ulisalia katika nchi hiyo ya Kiarabu kwa kisingizio cha kupambana na kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh miongo miwili baada ya kuivamia na kuikalia kwa mabavu nchi hiyo mwaka wa 2003, utaondoa kikamilifu wanajeshi wake ndani ya miaka miwili kuanzia sasa. Haya yameelezwa na Thabit al Abbasi Waziri wa Ulinzi wa Iraq.
-
Rais Pezeshkian wa Iran kuitembelea Iraq katika ziara ya kwanza nje ya nchi
Sep 08, 2024 11:35Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian anatazamiwa kuitembelea Iraq siku ya Jumatano katika safari yake ya kwanza ya nje tangu aingie madarakani.
-
Muqawama wa Iraq watumia droni za kamikaze kupiga Haifa
Sep 04, 2024 07:00Harakati ya Muqawama ya Iraq imefanya shambulizi la ndege zisizo na rubani dhidi ya mji wa Haifa, kaskazini mwa Palestina inayokaliwa kwa mabavu.
-
Muqawama Iraq kuanzisha tena operesheni dhidi ya majeshi ya US
Aug 26, 2024 12:19Makundi ya Muqawama ya kupambana na ugaidi ya Iraq yameafikiana kuanzisha tena operesheni dhidi ya kambi na vituo vya kijeshi vya Marekani katika nchi hiyo ya Kiarabu.
-
75% ya Waisrael wanaamini Netanyahu ameshindwa kukabiliana na Hizbullah
Aug 24, 2024 11:08Matokeo ya uchunguzi wa maoni uliofanywa na taasisi ya habari ya Mako ndani ya jamii ya Wazayuni yanaonyesha kuwa asilimia 75 ya Waisraeli hawaridhishwi na namna serikali ya waziri mkuu wa utawala huo Benjamin Netanyahu inavyoshughulikia hali ya usalama kwenye mpaka wa kaskazini, ambako kila siku kunaandamwa na mashambulio makali ya Harakati ya Muqawama wa Kiisilamu ya Hizbullah ya Lebanon tangu Israel ilipoanzisha vita dhidi ya Ukanda wa Ghaza Oktoba 7, 2023.
-
Muqawama Iraq: Jibu la Iran dhidi ya Israel litakuwa la nguvu
Aug 15, 2024 02:46Mkuu wa Baraza la Kisiasa la Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya al-Nujabaa ya Iraq amesema jibu tarajiwa la Iran kwa mauaji ya kigaidi yaliyofanywa mwezi uliopita na utawala wa Kizayuni dhidi ya Ismail Haniyah, Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS litakuwa la nguvu, lenye taathira na la kimahesabu.
-
Ayatullah Khamenei: Kipaumbele muhimu ni utekelezaji wa makubaliano kati ya Iran na Iraq
Jul 31, 2024 03:36Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema katika mazungumzo yake na Waziri Mkuu wa Iraq kwamba utekelezwaji wa mapatano baina ya nchi hizo mbili ndio kipaumbele muhimu zaidi.
-
Duru mpya ya mazungumzo ya pamoja ya usalama kati ya Marekani na Iraq mjini Washington
Jul 24, 2024 11:14Alina Romanowski, balozi wa Marekani mjini Baghdad, alitangaza siku ya Jumatatu kuhusu kuanza mazungumzo kati ya Marekani na Iraq huko Washington mji mkuu wa Marekani ajenda kuu ikiwa ni "mustakabali wa muungano wa kimataifa."
-
Iran iko tayari kushirikiana katika mapambano dhidi ya magendo ya madawa ya kulevya
Jul 24, 2024 02:37Waziri wa Mambo ya Ndani wa Iran amesema katika kikao cha Mkutano wa Pili wa Kikanda wa Kupambana na Madawa ya Kulevya huko Baghdad kuwa: Jamhuri ya Kiislamu ya Iran iko tayari kikamilifu kushirikiana na taasisi na mifumo ya kikanda na kimataifa kuendesha vita dhidi ya mihadarati.
-
Vikosi vya Yemen na Iraq vyafanya operesheni za kuitetea Palestina
Jul 16, 2024 07:18Vikosi vya wanamaji na vya makombora vya Yemen vimefanya operesheni nyingine dhidi ya meli za mafuta zilizokuwa zikielekea katika bandari za utawala wa Kizayuni unaokalia ardhi za Palestina kwa mabavu.