75% ya Waisrael wanaamini Netanyahu ameshindwa kukabiliana na Hizbullah
(last modified 2024-08-24T11:08:11+00:00 )
Aug 24, 2024 11:08 UTC
  • 75% ya Waisrael wanaamini Netanyahu ameshindwa kukabiliana na Hizbullah

Matokeo ya uchunguzi wa maoni uliofanywa na taasisi ya habari ya Mako ndani ya jamii ya Wazayuni yanaonyesha kuwa asilimia 75 ya Waisraeli hawaridhishwi na namna serikali ya waziri mkuu wa utawala huo Benjamin Netanyahu inavyoshughulikia hali ya usalama kwenye mpaka wa kaskazini, ambako kila siku kunaandamwa na mashambulio makali ya Harakati ya Muqawama wa Kiisilamu ya Hizbullah ya Lebanon tangu Israel ilipoanzisha vita dhidi ya Ukanda wa Ghaza Oktoba 7, 2023.

Kwa mujibu wa uchunguzi huo mpya wa maoni, ni asilimia 18 tu ya Waisraeli wanaamini kuwa serikali inasimamia vizuri hali ya usalama huko kaskazini kwenye mpaka wa pamoja na Lebanon.
 
Uchunguzi huo uliofanywa na Mako unaonyesha pia kuwa, zaidi ya nusu (asilimia 55) ya Waisraeli walmesema wanaamini uchaguzi mpya inapasa uitishwe hivi sasa hivii, huku asilimia 36 pekee wakisema serikali ya sasa inapasa iendelee kubaki mdarakani.
Netanyahu

Aidha, jumla ya asilimia 59 ya waliohojiwa wameonyesha kuunga mkono kufikia makubaliano na harakati ya Hamas ili kuwarejesha nyumbani mateka wa Israel, ikilinganishwa na asilimia 21 tu waliosema wanapinga mpango huo katika hali yake ya sasa, na wengine asilimia 20 ambao wamesema hawajui nini hasa kifanyike.

 
Matokeo ya uchunguzi huo wa maoni uliofanywa na Mako yanaonyesha pia kuwa 50% ya Waisraeli wanaamini kuwa waziri mkuu wa utawala huo wa Kizayuni Benjamin Netanyahu anachochewa na matashi ya kisiasa katika hatua anazochukua kwa ajili ya kuwarejesha nyumbani mateka wa Israel wanaoshikiliwa huko Ghaza.../

 

Tags