-
Kabila afuta gwaride la maadhimisho ya uhuru DRC kutokana na uasi jeshini
Jun 30, 2018 21:14Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo alifuta gwaride la jeshi katika maadhimisho ya mwaka wa 58 wa uhuru kutokana na kuwepo tetesi za uasi jeshini.
-
Jumamosi, Juni 30, 2018
Jun 29, 2018 23:31Leo ni Jumamosi tarehe 16 Mfunguo Mosi Shawwal 1439 Hijria mwafaka na tarehe 30 Juni 2018 Miladia.
-
UN: Pande zote Congo DR zimefanya jinai za kivita katika mkoa wa Kasai
Jun 26, 2018 11:22Wakaguzi wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa wametangaza kuwa jeshi la serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na makundi ya waasi yamefanya uhalifu unaofikia jinai za kivita na jinai dhidi ya binadamu ikiwa ni pamoja na kuua raia na kunajisi na kubaka wanawake na watoto.
-
DRC kumpa Bemba pasipoti ya kidiplomasia, kumruhusu arejee nyumbani
Jun 24, 2018 02:54Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imesema itampa pasipoti ya kidiplomasia Makamu wa Rais wa zamani wa nchi hiyo ambaye Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC ilimuondoa hatiani hivi karibuni.
-
Bunge la DRC kujadili sheria ya kuwalinda marais wa zamani
Jun 17, 2018 02:42Bunge la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo litakutana katika kikao maalumu, kufuatia ombi la Rais Joseph Kabila, kwa lengo la kujadili sheria ya kuwapa kinga ya kisheria marais wa zamani wa nchi hiyo.
-
Bemba awasili nchini Ubelgiji baada ya kuachiwa huru na ICC
Jun 16, 2018 02:51Aliyekuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Jean-Pierre Bemba, ambaye Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC siku chache zilizopita ilimuondoa hatiani kuhusu jinai za kivita, amewasili nchini Ubelgiji baada ya kuachiliwa huru na mahakama hiyo.
-
WHO: Ebola inatishia maisha ya watu Congo DR
Jun 13, 2018 11:06Shirika la Afya Dunia (WHO) limetahadharisha kuhusu maambukizi ya ugonjwa wa Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
-
Kabila wa DRC afuata nyayo za Nkurunziza, asema hatagombea muhula wa tatu wa urais
Jun 13, 2018 02:38Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo amesema Rais Joseph Kabila wa nchi hiyo hatagombea muhula wa tatu wa urais katika uchaguzi unaotazamiwa kufanyika baadaye mwaka huu.
-
Bemba wa DRC atakama mahakama ya ICC imuachilie baada ya kuondolewa hatiani
Jun 12, 2018 09:24Mawakili wa Jean-Pierre Bemba, makamu wa zamani wa rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ambaye Mahakama ya Kimataifa ya Jinai wiki iliyopita ilimuondoa hatiani kuhusu jinai za kivita, leo ametaka mahakama hiyo imuachilie huru.
-
Wakongomani wanaoishi nje ya nchi watakosa fursa ya kupiga kura katika uchaguzi ujao wa rais
Jun 10, 2018 12:20Baraza la taifa la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, limesema raia wa nchi hiyo wanaoishi nje ya nchi hawatopiga kura katika uchaguzi ujao wa rais.