-
Wasiwasi wa kuongezeka idadi ya wakimbizi DRC, wazidi kuwa mkubwa
May 21, 2017 03:11Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa, makumi ya maelfu ya watu wamekimbia makazi yao katikati mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na kukimbilia kusini mwa nchi hiyo.
-
Umoja wa Mataifa wakosoa kunyongwa watu DRC bila kufikishwa mahakamani
May 19, 2017 23:32Umoja wa Mataifa umekosoa ongezeko la vitendo vya kuwanyonga watu bila kuwapandisha mahakamani na ukiukaji wa haki za binaadamu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
SAUTI: Polisi ya Kinshasa yawabembeleza wakazi wa mji huo kuwataja wafungwa waliotoroka jela kuu, nao uvamizi wa jela wakikithiri
May 19, 2017 13:41Polisi ya mji wa Kinshasa, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imewataka wakazi wa mji huo kuisaidia serikali katika kuwataja wafungwa waliotoka jela kuu ya jiji hilo.
-
Jeshi la DRC laangamiza ngome ya wanamgambo wa Mai-Mai
May 17, 2017 09:19Mapigano makali yameripotiwa kutokea baina ya jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na wanamgambo wa Mai-Mai katika mkoa wa Kivu Kusini ulioko mashariki mwa nchi hiyo ambapo jeshi limefanikiwa kuangamiza ngome moja ya waasi hao.
-
Wimbi la wakimbizi wa CAR lamiminika nchini DRC
May 17, 2017 03:03Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa anayehusiana na wakimbizi ametangaza habari ya kumiminika maelfu ya wakimbizi wa Jamhuri ya Afrika ya Kati katika nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Walioambukizwa Ebola waongezeka DRC, wafika 20
May 16, 2017 09:52Nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC idadi ya visa vinavyoshukiwa kuwa ni Ebola imeongezeka na kufikia 20.
-
Mamia wauawa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
May 16, 2017 03:42Mamia ya watu wameripitiwa kuuawa katika mapigano makali baina ya wanamgambo wabeba silaha na askari wa serikali yaliyoibuka kuanzia mwishoni mwa mwezi Machi mwaka huu hadi sasa huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
SAUTI: Viongozi wa chama cha UDPS Kongo DR wawekwa kizuizini na polisi siku tatu, kuwazuia kujadili kuurejesha mwili wa Tshisekedi
May 13, 2017 14:07Huku mgogoro juu ya suala la kusafirishwa, kuagawa na kuzikwa kwa mwili wa mzee Étienne Tshisekedi kiongozi wa upinzani wa chama cha The Union for Democracy and Social Progress huko Kongo DR, ukiendelea kutokota, jeshi la polisi limewaweka kizuizini kwa siku tatu viongozi wa chama hicho.
-
Watuhumiwa wa mauaji Kongo DR wahukumiwa vifungo jela
May 13, 2017 09:18Mahakama ya kijeshi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imetoa adhabu ya kifungo cha maisha jela dhidi ya watu sita kwa kuhusika na mauaji na kushirikiana na makundi ya uhalifu, kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.
-
Ugonjwa wa Ebola waripotiwa DRC, watu watatu wafariki dunia
May 13, 2017 02:41Shirika la Afya Duniani (WHO) limetangaza kuwa, ugonjwa wa Ebola umezuka katika maeneo ya kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na kwamba, hadi sasa watu watatu wamefariki dunia kwa ugonjwa huo hatari.