-
Serikali ya DRC yawaachia huru wanaharakati wa upinzani
Dec 28, 2016 10:40Polisi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imewaachia huru wanaharakati wa upinzani waliokamatwa hivi karibuni katika maandamano dhidi ya serikali ya Rais Joseph Kabila wa nchi hiyo.
-
Makumi ya raia wauawa na wanamgambo wa ADF-Nalu Kongo DR
Dec 26, 2016 13:07Makumi ya raia wanaripotiwa kuuawa kufuatia mashambulio ya wanamgambo wa ADF-Nalu wa Uganda katika mkoa wa Kivu Kaskazini katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Raia 13 wauawa DRC mkoani Kivu katika hujuma ya kikabila
Dec 25, 2016 12:23Raia 13 wa kabila la Hutu wameuawa leo mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo katika kile kilichotajwa kuwa ni hujuma ya kulipiza kisasi iliyofanywa na wanagambo wa kabila la Nande.
-
Mazungumzo ya kuutafutia ufumbuzi mgogoro wa DRC yanaendelea
Dec 24, 2016 11:41Mazungumzo ya kuutafutia ufumbuzi mgogoro wa kisiasa wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo yameendelea huku wapinzani wakiendelea kushikilia msimamo wao wa kuondoka madarakani Rais Joseph Kabila.
-
Wapinzani DRC watoa sharti la kukubali muafaka wa kisiasa
Dec 24, 2016 04:15Wapinzani katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wametoa sharti ambalo wanasema lazima upande wa serikali ulikubali ili waunge mkono muafaka hafifu wa kisiasa uliofikiwa jana.
-
Mgogoro wa kisiasa Kongo DR wapatiwa ufumbuzi?
Dec 23, 2016 12:54Katika hatua ya ghafla na ambayo haikutazamiwa na wengi, pande hasimu za kisiasa katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo zimefikia muafaka, ambao utapelekea Rais Joseph Kabila asalie uongozini hadi mwishoni mwa mwaka ujao 2017.
-
Polisi Kongo yawatia mbaroni makumi ya raia
Dec 23, 2016 04:12Polisi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wamewatia mbaroni makundi ya raia kwa kosa la kushiriki maandamano dhidi ya serikali.
-
Hali yazidi kuwa tete DRC, 52 wauawa katika maandamano, mapigano ya kikabila
Dec 22, 2016 13:30Hali ya mambo katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imezidi kuwa tete huku makumi ya watu wakiuawa katika maandamano na mapigano ya kikabila.
-
Ban atoa wito kwa pande zote DRC kusuluhisha mgogoro kwa amani
Dec 22, 2016 04:33Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anayeondoka Ban Ki-moon ametoa wito kwa pande zote zinazohusika katika mgogoro wa kisiasa huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kutatua mgogoro huo kwa njia za amani.
-
Hali ya kulegalega kisiasa katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo
Dec 21, 2016 09:52Sambamba na kumalizika muhula wa kisheria wa uongozi wa Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, mji mkuu Kinshasa na miji mingine ya nchi hiyo imeshuhudia taswira ya kuimarisha usalama karibu katika kila kona.