-
Rais Pezeshkian: Umwagaji damu za maelfu ya watu wasio na hatia Lebanon hautabaki bila majibu
Sep 25, 2024 03:37Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuwa, jinai za kiholela na za kigaidi zilizofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel katika siku zilizopita na uchokozi wake mkubwa dhidi ya Lebanon ambao umemwaga damu za maelfu ya watu wasio na hatia hautabaki bila majibu.
-
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kukurubisha Madhehebu za Kiislamu ataka kusitishwa mauaji ya halaiki ya utawala wa Kizayuni
Sep 25, 2024 02:33Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Kukurubisha Madhehebu za Kiislamu amelaani jinai za hivi karibuni za utawala wa Kizayuni huko Lebanon na kutaka kuwepo na uungaji mkono wa nchi za Kiislamu na serikali zinazotetea amani na usalama duniani kwa ajili ya kusitisha mauaji ya kimbari yanayofanywa na Israel.
-
Ayatullah Sistani: Ichukuliwe hatua haraka kukomesha uchokozi wa Israel dhidi ya Lebanon
Sep 24, 2024 11:11Kiongozi wa juu wa kidini na Marjaa-Taqlidi wa Waislamu wa madhehebu ya Shia nchini Iraq Ayatullah Ali al-Sistani ameelezea mshikamano wake na Lebanon wakati nchi hiyo ya Kiarabu na Kiislamu inaendelea kuandamwa na mashambulio ya kinyama ya jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel na ametaka zifanyike juhudi za dharura kusitisha uchokozi huo wa kikatili wa utawala huo na kuwalinda raia wa Lebanon.
-
Profesa Fraihat: Vita vya Lebanon ni vya tatu vinavyofadhiliwa na serikali ya Biden
Sep 24, 2024 11:06Ibrahim Fraihat, Profesa wa Taaluma ya Usuluhishi wa Mizozo ya Kimataifa katika Taasisi ya Doha ya Mafunzo ya Wahitimu, amesema kupanuka kwa vita vilivyoanzishwa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Ukanda wa Ghaza hadi Lebanon kulitarajiwa, lakini kile ambacho hakikutarajiwa ni idadi kubwa ya vifo ndani ya muda wa siku moja.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Uingereza: Vita vya Ukraine vinaweza vikavuka mwaka 2026
Sep 24, 2024 11:02Waziri wa Mambo ya Nje wa Uingereza, David Lammy ametabiri kuwa mapigano kati ya Russia na Ukraine huenda yakaendelea kwa angalau miaka miwili zaidi na kuvuka mwaka 2026.
-
Nabih Berri atahadharisha kuhusu hulka ya kupenda vita ya utawala wa Kizayuni katika eneo
Sep 23, 2024 12:02Spika wa bunge la Lebanon ameashiria kuendelea mashambulizi ya utawala wa Kizayuni nchini humo na kusema, Benjamin Netanyahu Waziri Mkuu wa utawala huo anafanya kila awezalo ili kuitumbukiza Lebanon na eneo hili katika vita vikubwa.
-
UN yapitisha Mkataba wa Zama Zijazo (Pact for the Future), Guterres: Sasa ni wakati wa vitendo
Sep 23, 2024 07:09Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limepitisha Mkataba wa Zama Zijazo (Pact for the Future) baada ya vuta nikuvute zilizokuwepo ambapo Katibu Mkuu wa umoja huo Antonio Guterres ameshukuru wawezeshaji wote waliojitolea kufanikisha kupitishwa kwa mkataba huo adhimu.
-
Kan'ani: Marekani ndiyo inayopaswa kubeba dhima ya jinai za Israel huko Palestina, Lebanon na Syria
Sep 22, 2024 02:59Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya ya Iran amesema kuwa, Marekani ndiyo inayopaswa kubeba dhima na kujibu malalamiko makubwa ya kimataifa kwa kushiriki kwake katika jinai za utawala wa Kizayuni huko Palestina, Lebanon na Syria.
-
Data za Waindonesia milioni sita akiwemo Rais na wanawe zavujishwa na kuuzwa tovutini
Sep 20, 2024 06:51Data za walipakodi milioni sita katika taifa la nne kwa idadi kubwa zaidi ya watu duniani, Indonesia, zikiwemo za Rais anayemaliza muda wake Joko Widodo, zimedaiwa kuvujishwa na kuuzwa. Hayo ni kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa na vyombo vya habari jana Alkhamisi.
-
Onyo la UN kuhusu matumizi mabaya ya zana za kiraia kwa madhumuni ya kigaidi
Sep 20, 2024 02:30Kufuatia wimbi kubwa la milipuko ya kigaidi nchini Lebanon ambayo imelenga vifaa vya mawasiliano kama vile pager, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema vifaa vya kiraia havipaswi kugeuzwa kuwa silaha.