-
Vita vya Ethiopia na jitihada za kutatua mgogoro wa nchi hiyo
Jan 13, 2022 00:51Wakati maafisa wa serikali ya Ethiopia wakiahidi kuanzisha mazungumzo ya kitaifa nchini humo, Harakati ya Ukombozi wa Watu wa Tigray (TPLF) imetangaza kuwa mashambulizi ya jeshi la Ethiopia katika eneo hilo yamesababisha vifo vya zaidi ya raia 56.
-
Waziri Mkuu wa Ethiopia kuingia katika medani ya vita kukabiliana na TPLF
Nov 23, 2021 04:05Abiy Ahmed, Waziri Mkuu wa Ethiopia ametangaza kuwa leo atajitosa kwenye medani ya vita kati ya vikosi vya serikali ya nchi hiyo na wapiganaji wa Harakati ya Ukombozi ya Watu wa Tigray (TPLF).
-
Watu zaidi ya 51 wauawa katika hujuma ya magaidi nchini Mali
Aug 10, 2021 03:10Zaidi ya watu 51 wameuawa katika hujuma iliyofanyika kaskazini mwa Mali karibu na mpaka wa nchi hiyo na Niger.
-
Mazungumzo ya amani yaanza baina ya serikali ya Sudan na waasi wa SPLM huko Juba
May 26, 2021 21:51Mazungumzo ya amani baina ya serikali ya Sudan na Harakati ya Ukombozi wa Watu wa Sudan tawi la Kaskazini (SPLM) yalianza jana katika mji wa Juba chini ya usimamizi wa Rais ya serikali ya Sudan Kusini, Salva Kiir Mayardit.
-
Yafichuka: Mossad imehusika katika jaibio la mapinduzi nchini Jordan
Apr 05, 2021 08:25Tovuti ya Axios ya Marekani imefichua kuwa, shirika la ujasusi la Israel, MOSSAD, limehusika katika jaribio la mapinduzi lililofanyika nchini Jordan.
-
UN yabainisha wasiwasi wake kuhusu kuongezeka mapigano huko al Hudaydah, Yemen
Jan 28, 2021 22:37Umoja wa Mataifa umesema kuwa, una wasiwasi kutokana na kuongezeka mapigano kati ya wapiganaji wa harakati ya Ansarullah na wale wa serikali iliyojiuzulu ya Yemen katika eneo la kistratejia la al Hudaydah.
-
Mamluki wa Saudia na Imarati wazidi kutwangana nchini Yemen
Nov 28, 2020 06:58Mapigano makali yanaendelea kusini mwa Yemen, baina ya mamluki wa Saudi Arabia chini ya serikali iliyojiuzulu ya Mansour Hadi na mamluki wa Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati), chini ya Baraza la Mpito la Kusini.
-
UNHCR: Maelfu ya Waethiopia wanaendelea kuelekea Sudan
Nov 19, 2020 03:28Shirika la Wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR) limetangaza kuwa, vita vinavyoendela katika eneo la Tigray baina ya jeshi la serikali ya Ethiopia na wapiganaji wa Harakati ya Ukombozi wa Watu wa Tigray (TPLF) vimewalazimisha raia karibu elfu 30 kukimbilia nchi jirani ya Sudan.
-
Wafuasi na wapinzani wa Trump wapigana Washington, Marekani
Nov 15, 2020 04:39Maandamano ya wafuasi wa rais wa Marekani, Donald Trump mjini Washington DC yameingia kwenye machafuko baada ya kuzuka mapigano baina yao na watu wanaopinga ubaguzi wa rangi.
-
Wapiganaji wa Janjaveed wa Sudan wapelekwa Libya kujiunga na Haftar
Aug 11, 2020 06:53Jeshi la Serikali ya Mwafaka wa Kitaifa nchini Libya limetangaza kuwa mfasara uliokuwa na magari 70 ya kijeshi yakibeba silaha na mamluki wa kundi la Janjaweed umevuka maeneo maarufu kama Hilali ya Mafuta ya Libya ukiuelekea katika mji wa Sirte kwa ajili ya kumsaidia jenerali muasi, Khalifa Haftar.