-
Wananchi wa Morocco waandamana kuwaunga mkono Wapalestina wa Gaza
Nov 08, 2023 03:40Wananchi wa Morocco kwa mara nyingine tena wamefanya maandamano ya kuwanga mkono wananchi wa Palestina ambao wanakabiliwa na hujuma na mashambulizi ya kikatili ya utawala haramu wa Israel katika Ukanda wa Gaza.
-
Rais wa Iran: Kuendelea kwa mauaji ya Wapalestina kutaathiri ulimwengu
Nov 07, 2023 04:47Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema Tehran inaunga mkono juhudi za pamoja za kimataifa kwa ajili ya usitishaji vita mara moja, kuondoa mzingiro na kutoa misaada kwa watu wanaodhulumiwa wa Ghaza na kusisitiza kuwa: Mauaji ya watu wa Palestina yameyakasirisha mataifa yote huru duniani, na kuendelea kwa mauaji haya kutakuwa na matokeo mabaya hadi nje ya kanda ya Magharibi mwa Asia.
-
Maandamano ya kuwaunga mkono Wapalestina yafanyika Ujerumani, Italia
Nov 05, 2023 10:11Maelfu ya watu wamejitokeza mabarabarani katika mji mkuu wa Ujerumani, Berlin kushiriki maandamano ya kulaani jinai zinazoendelea kufanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya wananchi wa Palestina, huku idadi ya Wapalestina waliouawa shahidi hadi sasa katika mashambulizi dhidi ya Ukanda wa Gaza ikipindukia 10,000.
-
Mpira wa kusimamisha au kupanua wigo wa vita Ghaza uko katika uwanja wa Netanyahu na jeshi la Kizayuni
Nov 05, 2023 03:22Operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa inakaribia kufika mwezi mmoja tangu itekelezwe huku jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel likiendelea kuwaua watu wa Ghaza na kujaribu kufidia kushindwa kwao katika vita vya nchi kavu kwa kuwaua raia kwa umati.
-
Balozi wa Cuba: Israel ndiye gaidi halisi
Nov 03, 2023 23:32Balozi wa Cuba mjini Tehran sanjari na kulaani jinai za Israel dhidi ya wananchi wa Palestina katika Ukanda wa Gaza, ameutaja utawala huo wa Kizayuni wa Israel kuwa utawala wa kigaidi.
-
"Vita vya Israel dhidi ya Gaza vinafanana na vita vya Saddam dhidi ya Iran"
Nov 03, 2023 08:59Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema mashambulizi yasiyo na kikomo ya utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza yanashabihiana na vita vya kivamizi na kichokozi vya dikteta wa zamani wa Iraq, Saddam Hussein dhidi ya Iran katika miaka ya 1980.
-
Wapalestina sasa wazika mashahidi wao katika makaburi ya umati
Nov 03, 2023 08:58Habari kutoka Ukanda wa Gaza zinaarifu kuwa, kutokana na kushtadi mashambulizi ya kinyama ya utawala haramu wa Israel na kuongezeka kwa kiwango cha kutisha idadi ya wananchi wa Palestina wanaouawa shahidi katika eneo hilo, Wapalestina hivi sasa wanalazimika kuwazidi mashahidi wao katika makaburi ya halaiki.
-
Maangamizi ya kizazi Ukanda wa Ghaza na ubinadamu uliotoweka katika nchi za Magharibi
Nov 02, 2023 05:40Ni wakati mwingine wa kuwa nanyi wapenda wasikilizaji katika Makala ya Wiki hii na leo tutazungumzia maangamizi ya kizazi katika eneo la Ukanda wa Ghaza na kuporomoka kwa ubinadamu katika nchi za Magharibi.
-
Kuendelea uungaji mkono wa nchi za Magharibi kwa utawala wa Kizayuni; miaka 106 baada ya Azimio la Balfour
Nov 01, 2023 22:49Tarehe 2 Novemba 2023 inaambatana na maadhimisho ya miaka 106 ya Azimio maarufu la Balfour.
-
"Okoa watoto wa Gaza", Wamarekani wakatiza kikao cha Kongresi cha kumsaili Blinken na Austin
Nov 01, 2023 04:45Waandamanaji jana Jumanne walikatiza kikao cha kuwahoji mawaziri wa Mambo ya Nje na Ulinzi wa Marekani katika Bunge la Kongresi kilichoitishwa kwa ajiili ya kijadili suala la kuongeza uungaji mkono na misaada kwa Israel na Ukraine. Waandamanaji hao walioingia ndani ya Kongresi walitoa nara wakitaka "kuokolewa watoto wa Gaza" na "kusitishwa mapigano mara moja" katika eneo hilo la Palestina.