-
Umaskini waongezeka sana Ukanda wa Ghaza
Jan 08, 2017 10:13Kituo cha Haki za Binadamu cha Palestina kimetangaza habari ya kuongezeka umaskini kwa asilimia 65 katika eneo la Ukanda wa Ghaza kutokana na kuendelea kuzingirwa kiuchumi kikamilifu eneo hilo na utawala wa Kizayuni.
-
Hatua ya Israel ya kuuzuia ujumbe wa ICC kuingia Ukanda wa Gaza
Oct 10, 2016 04:06Ujumbe kutoka ofisi ya Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) siku ya Jumamosi uliwasili katika ardhi za Palestina zilizovamiwa na kuanza kukaliwa kwa mabavu mwaka 1948 (Israel). Ujumbe huo umepangiwa kutembelea pia eneo la Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan, lakini hautofika Ukanda wa Gaza baada ya Israel kuuzuia kufanya hivyo.
-
Israel yawateka nyara wanaharakati wanawake wakielekea Gaza
Oct 06, 2016 12:16Jeshi la majini la utawala wa Kizayuni wa Israel limewateka nyara wanaharakati wanawake wa Marekani akiwemo Ann Wright, mwanadiplomasia mashuhuri na mtetezi wa haki za binadamu, wakiwa kwenye boti wakielekea katika Ukanda wa Gaza.
-
Misri yafungua tena kivuko cha Rafah kwa muda
Jun 29, 2016 09:12Misri imefungua tena kivuko cha Rafah, njia pekee inayotumiwa kufikishia misaada ya dharura kwa Wapalestina karibu milioni mbili walio chini ya mzingiro huko Ukanda Gaza tangu mwaka 2007 na kusema kuwa eneo hilo la mpakani litasalia wazi hadi Julai 4.
-
Ban: Israel inawaumiza Wapalestina kwa mzingiro wake Ghaza
Jun 28, 2016 23:56Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-moon amelaani mzingiro wa Israel huko Ukanda wa Ghaza na kusema unawaumiza Wapalestina na kuharibu uchumi wao.
-
Mzingiro wa Israel wawafanya watoto Gaza waache masomo na kulazimika kufanya kazi
Jun 12, 2016 03:13Idadi kubwa ya watoto wa Kipalestina katika Ukanda wa Gaza wamelazimika kuacha masomo na kufanya kazi ili kuzisaidia familia zao kimaisha kutokana na dhiki iliyosababishwa na mzingiro na mashambulio ya kijeshi ya utawala wa Kizayuni dhidi ya eneo hilo.
-
Wiki ya kimataifa ya kuondoa mzingiro wa Ukanda wa Gaza
Jun 06, 2016 06:44Wakati maadhimisho ya kimataifa ya kuondoa mzingiro uliowekewa Ukanda wa Gaza yakiwa yanakaribia, A'laa al-Batt'ah, mratibu wa harakati za kitaifa za kuondoa mzingiro wa Gaza ametoa wito kwa Wapalestina na watetezi wa uhuru duniani kote kushiriki katika shughuli na harakati za wiki ya kimataifa ya kuondolewa mzingiro wa Gaza ambayo inatazamiwa kuanza katika wiki ya mwisho ya mwezi huu wa Juni.
-
Asilimia 97 ya maji ya Ukanda wa Gaza si safi na si salama
May 18, 2016 03:30Idara ya Maji ya Palestina imetangaza kuwa zaidi ya asilimia 97 ya maji ya Ukanda wa Gaza hayafai kutumiwa kwa kunywa.
-
Hamas: Hujuma mpya ya Israel Ukanda wa Gaza itapata jibu kali
May 06, 2016 23:50Naibu Mkuu wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina (HAMAS) ameuonya Utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya mashambulizi yake mapya katika Ukanda wa Gaza huku uvamizi huo mpya wa Tel Aviv katika eneo hilo ukiingia siku yake ya nne Jumamosi.
-
Jeshi la Israel laanzisha mashambulizi dhidi ya kambi za Hamas, Gaza
May 04, 2016 22:14Jeshi la utawala wa kizayuni wa Israel limeshambulia kwa makombora minara ya kijeshi inayomilikiwa na harakati ya mapambano ya Kiislamu ya Palestina Hamas katika Ukanda wa Gaza.