-
Seneta wa Nigeria: Jinai za Israel Gaza, Lebanon zinaonyesha UN haina maana
Sep 27, 2024 03:05Mwanasiasa wa ngazi ya juu wa Nigeria amesema kuwa, mauaji ya kimbari ya Israel dhidi ya raia wa Palestina katika Ukanda wa Gaza na huko Beirut, mji mkuu wa Lebanon yameonyesha kushindwa kwa dunia kushughulikia suala la Palestina, na pia imeonyesha namna Umoja wa Mataifa ulivyo butu kwa kushindwa kukomesha ukatili na unyama wa Israel.
-
UN yapitisha Mkataba wa Zama Zijazo (Pact for the Future), Guterres: Sasa ni wakati wa vitendo
Sep 23, 2024 07:09Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limepitisha Mkataba wa Zama Zijazo (Pact for the Future) baada ya vuta nikuvute zilizokuwepo ambapo Katibu Mkuu wa umoja huo Antonio Guterres ameshukuru wawezeshaji wote waliojitolea kufanikisha kupitishwa kwa mkataba huo adhimu.
-
Russia: Azimio la Umoja wa Mataifa linaweka wazi uharamu wa vitendo vya Israel
Sep 20, 2024 12:42Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia imetangaza kuwa, azimio jipya la Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ni hatua muhimu ambayo inaiwezesha jamii ya kimataifa kutambua uharamu wa hatua za Israel.
-
Askari wa Israel waziporomosha kwa mateke maiti za Wapalestina kutokea kwenye paa la jengo
Sep 20, 2024 07:40Askari katili wa jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel wamedhihirisha tena unyama wao baada ya kunaswa kupitia mkanda wa video wakiziporomosha kwa mateke maiti za Wapalestina waliowaua katika shambulio walilofanya katika eneo la Qabatiya, Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan unaokaliwa kwa mabavu.
-
Katibu Mkuu wa UN atoa indhari kuhusu hatari ya Akili Mnemba (AI)
Sep 15, 2024 12:10Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres ametoa indhari kuhusu Akili Mnemba au Bandia (Artifcial Intelligence) na kusisitiza kuwa endapo itaachwa bila kudhibitiwa, hatari inazosababisha zinaweza kuwa na athari kubwa kwa demokrasia, amani na utulivu.
-
Mashirika ya haki za binadamu yataka UN 'iwalinde' mateka wa Kipalestina
Sep 13, 2024 02:32Mashirika ya kutetea haki za binadamu yametoa wito kwa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa kuchukua hatua za haraka "kuwalinda watu walionyimwa uhuru wao" katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu.
-
Mkuu wa haki za binadamu wa UN awakosoa wanasiasa kwa kukandamiza haki za binadamu
Sep 10, 2024 07:17Mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa jana alifungua kikao cha 57 cha Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa mjini Geneva Uswisi na kuzungumzia masuala mbalimbali yanayoisibu dunia ikiwemo machafuko ya kisiasa, kukandamizwa haki za wanawake na uhuru wa vyombo vya habari na kujieleza.
-
Takwa la Umoja wa Mataifa la kuwekewa vikwazo Israel
Sep 09, 2024 13:06Ripota maalumu wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki ya chakula amesema kuwa, Israel sio tu inazuia misaada ya kibinadamu kuingia Gaza, bali pia inaharibu ardhi na vyanzo vya chakula vya Palestina.
-
Sudan yapinga ripoti ya Umoja wa Mataifa, yasema ni ya kisiasa
Sep 08, 2024 12:03Sudan imekadhibisha ripoti mpya ya Jopo Huru la Umoja wa Mataifa la Kutafuta Ukweli, ambayo inazituhumu pande zinazozozana nchini humo kwa kufanya ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu ambao unaweza kuwa uhalifu wa kivita.
-
Kifo cha Mmarekani Mturuki kimedhihirisha unafiki na undumilakuwili wa Marekani
Sep 07, 2024 11:05Msimamo wa Marekani wa kutoa mijibizo tofauti kuhusiana na vifo vya raia wake waliouliwa na jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel na wale waliofariki katika matukio mengine umedhihirisha unafiki na undumilakuwili wa serikali ya Washington.