-
Uganda yadondosha msaada wa chakula Sudan Kusini
Jun 01, 2025 06:38Jeshi la Uganda limetangaza kuwa limefanya zoezi la kudondosha tani 600 za chakula muhimu kwa ajili ya wakazi wa maeneo kadhaa ya jimbo lililokumbwa na ghasia la Upper Nile huko Sudan Kusini.
-
Waziri Mkuu mpya wa Sudan ala kiapo cha kikatiba
Jun 01, 2025 03:43Kamil Idris aliapishwa jana Jumamosi kuwa Waziri Mkuu mpya wa Sudan, mbele ya Abdel Fattah al-Burhan, Mkuu wa Baraza la Mpito linalotawala nchini humo.
-
Idadi ya waliofariki kutokana na mafuriko nchini Nigeria yaongezeka hadi 151
May 31, 2025 22:52Idadi ya waliofariki dunia kutokana na mafuriko makubwa kwenye mji wa Mokwa, wa kaskazini-kati mwa Jimbo la Niger nchini Nigeria, imepanda na kufikia hadi 151.
-
Afrika Kusini yaanza kuchunguza jinai za enzi za 'apartheid'
May 31, 2025 07:15Rais Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini amemteua Jaji mstaafu wa Mahakama ya Kikatiba, Sisi Khampepe kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Ukweli na Maridhiano (TRC) ya kuchunguza ucheleweshaji wa mashtaka na uchunguzi wa jinai zilizofanyika enzi za ubaguzi wa rangi (apartheid) nchini humo.
-
Jeshi la Nigeria laua magaidi 60 wa Boko Haram jimbo la Borno
May 31, 2025 06:51Jeshi la Nigeria limetangaza habari ya kuwaua wanachama 60 wa kundi la kigaidi la Boko Haram baada ya kuzima shambulio dhidi ya kambi ya kijeshi huko Bita, eneo la Gwoza, kaskazini mashariki mwa Jimbo la Borno.
-
Shambulio la droni la waasi wa RSF laua watu sita hospitalini Sudan
May 31, 2025 03:40Vikosi vya kijeshi vya Rapid Support Forces (RSF) vya Sudan vililishambulia jiji la El-Obeid siku ya Ijumaa kwa kutumia droni, na kuua watu sita katika hospitali moja muhimu kusini mwa nchi, kwa mujibu wa vyanzo vya kitabibu na kijeshi.
-
Mafuriko yaua makumi ya watu nchini Nigeria
May 30, 2025 22:51Makumi ya watu wamepoteza maisha huku maelfu ya wengine wakilazika kuhama makazi yao kutokana na mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa zinazonyesha nchini Nigeria.
-
Magaidi wenye mfungamano na al-Qaeda waongeza mashambulio yao Msumbiji
May 30, 2025 07:20Wanamgambo wanaoaminika kuwa wanachama wa kundi la kigaidi linalojiita Ahlu Sunna Wal Jamaa (ASWJ) lenye mfungamano na mtandao wa al-Qaeda wameongeza mashambulio yao kaskazini mwa Msumbiji na kuzusha wasiwasi kwa mara nyingine.
-
Mwanamke Afrika Kusini afungwa maisha jela kwa kumuuza binti yake
May 30, 2025 04:02Mwanamke mmoja kutoka Afrika Kusini amehukumiwa kifungo cha maisha gerezani kwa kosa la kumuza binti yake mwenye umri wa miaka sita. Kwa mujibu wa nyaraka za mahakama, mtoto huyo aliyetambulika kwa jina la Joshlin Smith, aliuzwa kwa kiasi cha takribani dola 1,122 za Marekani (sawa na R20,000).
-
Milipuko ya kipindupindu yaongezeka Khartoum, Sudan
May 30, 2025 03:48Serikali ya Sudan imetangaza ongezeko kubwa la visa vya kipindupindu katika jimbo la Khartoum, ambapo kwa siku moja tu, visa 1,375 vipya vimeripotiwa, na vifo 23 kuthibitishwa.