-
WFP: Familia nchini Sudan zinapitia kipindi kigumu kufuatia mizozo ya kikatili, njaa na uhaba wa fedha
Jan 15, 2026 23:23Familia nchini Sudan zinasukumwa ukingoni huku "migogoro ya kikatili" na njaa vikiendelea. Mpango wa Chakula Duniani (WFP) pia umetahadharisha kuwa oparesheni zake za kibinadamu za kunusuru maisha ya wananchi wa Sudan zinasusua kufuatia uhaba mkubwa wa fedha.
-
ANC yaonya kuhusu njama za 'mapinduzi' nchini Iran
Jan 15, 2026 22:43Mkuu wa vuguvugu la Mshikamano wa Kimataifa wa chama tawala cha African National Congress (ANC) katika jimbo la Western Cape nchini Afrika Kusini ameonya kwamba, machafuko ya hivi karibuni nchini Iran yana mkono wa Marekani na washirika wake wa Kizayuni.
-
Magaidi 30 wa al-Shabaab wauawa na vikosi vya Somalia, Uganda na AU
Jan 15, 2026 22:43Vikosi vya Somalia, Uganda na Umoja wa Afrika (AU) jana Alhamisi viliwaangamiza zaidi ya wanamgambo 30 wa al-Shabaab, na kujeruhi wengine kadhaa wakati wa operesheni ya pamoja huko kusini mwa Somalia.
-
Misri: Umoja wa Sudan ni mstari mwekundu kwetu, hatutasita kuchukua kila hatua kuulinda
Jan 15, 2026 22:42Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri, Badr Abdelatty amesema, nchi yake itachukua hatua zote zinazohitajika ili kuhifadhi umoja wa ardhi ya Sudan, wakati nchi hiyo jirani inakaribia kuingia mwaka wake wa nne wa vita vya wenyewe kwa wenyewe vinavyohusisha vikosi vya jeshi SAF na vile vya usaidizi wa haraka, RSF.
-
Zoezi la kuhesabu kura nchini Uganda linaendelea
Jan 15, 2026 11:41Shughuli za kuhesabu kura zimeanza katika vituo mbalimbali vya kupigia kura kote Kampala na sehemu zingine za Uganda, baada ya kumalizika kwa zoezi la upigaji kura.
-
Maelfu ya Wanigeria wakimbia makazi yao baada ya kiongozi wa genge la waasi kutishia kuwaua
Jan 15, 2026 04:15Maafisa wa serikali na wakazi wa kaskazini magharibi mwa Nigeria wamesema kwamba maelfu ya watu wamekimbia makazi yao wiki hii baada ya kiongozi wa genge lenye silaha kuwaamuru waondoke kwenye maeneo hayo.
-
Kenya: Umaskini wasababisha zaidi ya wanafunzi laki 8 kukosa kuripoti shule
Jan 15, 2026 03:31Ripoti kutoka Kenya zinasema umaskini pamoja na hatua ya serikali kudhibiti uteuzi wa shule, umeibuka kuwa sababu kuu inayofanya zaidi ya wanafunzi 800,000 wa Gredi ya 10 kushindwa kuripoti katika shule walizoteuliwa.
-
Wananchi wa Uganda wanapiga kura leo, Museveni atarajiwa kuendelea kutawala
Jan 15, 2026 00:42Wananchi wa Uganda waliotimiza masharti ya kupiga kura, leo wanaelekea katika vituo vya kupigia kura kuamua hatiam ya uongozi wa nchi hiyo kwa miaka mingine mitano.
-
Indhari ya Hamas kuhusu hali mbaya ya kibinadamu Gaza
Jan 14, 2026 23:08Baada ya kufariki kwa idadi ya watoto wa Kipalestina katika Ukanda wa Gaza kutokana na baridi kali, Harakati ya Kiislamu ya Kupigania Ukombzoi wa Palestina, Hamas, imeonya kuhusu kuzidi kuzorota kwa hali ya kibinadamu katika eneo hilo ambalo liko chini ya mzingiro wa utawala katili wa Israel.
-
Mahakama ya Tunisia yaidhinisha kifungo cha miaka 22 dhidi ya kiongozi wa Ennahda, Ghannouchi
Jan 14, 2026 23:07Mahakama ya rufaa nchini Tunisia siku ya Jumatano imethibitisha kifungo cha miaka 22 jela dhidi ya Rached Ghannouchi, kiongozi wa Harakati ya Ennahda na aliyekuwa Spika wa Bunge, katika kesi maarufu ya Instalingo.