-
Mshauri wa IRGC auawa shahidi katika shambulio la anga lililofanywa na Israel nchini Syria
Feb 02, 2024 10:39Mshauri wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu IRGC ameuawa shahidi kufuatia shambulio la ndege za kivita za utawala wa Kizayuni katika mji wa Aqrabah kusini mwa mji mkuu wa Syria Damascus, karibu na eneo la Sayeda Zainab.
-
Khatibu wa Sala ya Ijumaa mjini Tehran: Iran ni nchi huru zaidi duniani
Feb 02, 2024 10:28Khatibu wa Sala ya Ijumaa iliyosaliwa leo mjini Tehran ameitaja Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kuwa nchi huru zaidi duniani.
-
Abdollahian: Kusitisha jinai za Israel ndiyo njia pekee ya kurejesha uthabiti Asia Magharibi
Feb 02, 2024 04:20Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema njia pekee ya kurejesha uthabiti katika eneo la Asia Magharibi ni kukomesha jinai za utawala wa Israel dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza.
-
Raisi: Visiwa 3 vya Ghuba ya Uajemi ni sehemu isiyotenganishika na Iran
Feb 01, 2024 23:29Rais wa Iran amesema visiwa vitatu vinavyomilikiwa na nchi hii vya Bu Musa, Tomb Ndogo na Tomb Kubwa katika Ghuba ya Uajemi daima vitasalia kuwa milki ya Jamhuri ya Kiislamu.
-
Spika ya Majlisi ya Iran: Utamaduni wa kufa shahidi unawatia hofu maadui
Feb 01, 2024 23:12Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (Bunge) ameeleza kuwa utamaduni wa kufa shahidi unawatia hofu maadui.
-
Kuanza Alfajiri Kumi za Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran
Feb 01, 2024 08:55Leo (Alhamisi), tarehe 12 Bahman 1402 Hijria Shamsia inayosadifiana na tarehe Mosi Februari 2024, ni mwanzo wa siku kumi zlizobarikiwa za alfajiri ya Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran.
-
"US inakiuka Hati ya UN kwa kutishia kuiwekea tena vikwazo Venezuela"
Feb 01, 2024 08:32Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amekosoa vikali hatua ya Marekani ya kutishia kuiwekea upya vikwazo sekta ya mafuta ya Venezuela na kusisitiza kuwa, kkitendo hicho kinakanyaga Hati ya Umoja wa Mataifa na sheria ya kimataifa.
-
Iran yaitaka Marekani iache kutumia lugha ya vitisho dhidi yake
Feb 01, 2024 07:45Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ameitaka Marekani iache kutumia lugha ya vitisho dhidi ya taifa hili na kusisitiza kuwa, vitisho vyovyote dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu vitakabiliwa na jibu madhubuti na la haraka.
-
Maadhimisho ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu yaanza rasmi nchini Iran
Feb 01, 2024 03:45Alkhamisi ya leo ya tarehe Mosi Februari 2024 inasadifiana na tarehe 12 Bahman 1402 kwa kalenda ya Iran ya Hijria Shamsia. Tarehe kama hii kila mwaka huwa ndio mwanzo wa maadhimisho ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya nchini Iran.
-
Mipaka ya Iran na Pakistan kubadilishwa kuwa ya kiuchumi na kiurafiki
Jan 31, 2024 23:29Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa, juhudi zinafanyika kuhakikisha kwamba, mipaka ya nchi yake na Pakistan inabadilika na kuwa ya kiuchumi, amani na urafiki.