-
Kiongozi Muadhamu: Kuna udharura wa kukatwa mishipa ya uhai ya utawala wa Kizayuni
Jan 23, 2024 10:01Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitiza kuwa: Nchi za Kiislamu zinapaswa kukata uhusiano wao wa kisiasa na kiuchumi na utawala wa Kizayuni wa Israel kwa kukata mishipa muhimu ya uhai ya utawala huo ghasibu.
-
Jeshi la Iran lapokea idadi kubwa ya ndege za kivita zisizo na rubani
Jan 23, 2024 09:45Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran limepokea idadi kubwa ya ndege za kivita zisizo na rubani zenye uwezo mkubwa wa vita vya kistratijia, upelelezi na pia baadhi zinaweza kutumika kama rada.
-
Amir-Abdollahian: Dhati ya kigaidi ya Israel imedhihirika kwa kuwaua washauri wa kijeshi wa Iran
Jan 23, 2024 03:54Kufuatia kuuawa shahidi washauri watano wa kijeshi wa Iran katika shambulio la kigaidi lililofanywa na jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel nchini Syria, Waziri wa Mambo ya Nje Hossein Amir-Abdollahian amemwandikia barua Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa na kueleza kwamba: hatua ya kigaidi ya Israel dhidi ya washauri wa kijeshi wa Iran imedhihirisha wazi dhati halisi ya kigaidi ya utawala huo.
-
Abdollahian: Uhusiano wa Iran na Algeria upo katika mazingira bora kabisa
Jan 23, 2024 00:52Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, uhusiano wa taifa hili na Algeria upo katika kiwango bora kabisa.
-
Wairani wajitokeza kwa wingi kuwaaga mashahidi wa shambulizi la kigaidi la Israel
Jan 22, 2024 08:38Shughuli ya kuwaaga mashahidi wa shambulizi la kigaidi la Israel nchini Syria imefanyika hapa Tehran kwa kuhudhuriwa na viongozi wa ngazi ya juu, familia za mashahidi hao na umati mkubwa wa wananchi Waislamu wa Iran.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran kuitembelea Misri karibuni
Jan 22, 2024 08:35Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Hossein Amir-Abdollahian anataziwa kuitembelea Misri ndani ya siku chache zijazo, huku utawala wa Kizayuni ukiingiwa na kiwewe kutokana na kuendelea kuimarika uhusiano wa Tehran na Cairo.
-
Satalaiti ya Thuraya; nembo nyingine ya uwezo mkubwa wa wasomi vijana wa Iran
Jan 22, 2024 05:38Satalaiti ya Thuraya ambayo imebuniwa na kutengenezwa kwa juhudi na hima ya wasomi vijana wa Iran na kurushwa katika anga za juu, imefanikiwa kutuma taarifa zake za awali na kuthibitisha kuwa imetua sehemu iliyokusudiwa kwa mafanikio makubwa.
-
Raisi: Iran inaunga mkono kesi ya Afrika Kusini dhidi ya Israel ICJ
Jan 22, 2024 04:01Rais wa Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu inaunga mkono uamuzi wa 'busara' na wa 'kihistoria' wa Afrika Kusini wa kuwasilisha kesi dhidi ya utawala haramu wa Israel katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ), kuhusu jinai za mauaji ya kimbari zinazotekelezwa na utawala huo dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza.
-
Satalaiti mpya ya Iran yatuma taarifa za kwanza kabisa ardhini
Jan 21, 2024 23:29Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuwa, satalaiti mpya zaidi ya Iran iitwayo Thuraya imefanikiwa kuunganisha mawasiliano ardhini na kutuma taarifa za awali kabisa.
-
Amir-Abdollahian: Harakati za washauri wa kijeshi wa Iran za kupambana na ugaidi zitaendelea kwa nguvu kamili
Jan 21, 2024 07:56Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ametoa mjibizo kufuatia kuuawa shahidi washauri watano wa Iran nchini Syria katika shambulio la kigaidi la utawala wa Kizayuni na kueleza kwamba: "kushindwa Wazayuni kukabiliana na irada na matakwa ya watu wa Gaza hakutaweza kufidiwa kwa vitendo hivi vya kigaidi."