-
Al Azhar yalaani jinai mpya za Wazayuni; Tunisia wamuunga mkono Sinwar
Aug 11, 2024 00:53Chuo Kikuu cha Kiislamu cha al Azhar cha Misri kimelaani vikali jinai mpya ya utawala wa Kizayuni ya kuwaua kikatili Waislamu waliokuwa wanasali katika kambi ya wakimibizi huko Ghaza na kusisitiza kuwa, maneno ya kuelezea jinai na ukatili mbaya mno wa Wazayuni, hayapatikani.
-
Muqawama: US ni mshiriki wa mauaji mapya ya halaiki Gaza
Aug 10, 2024 07:43Makundi ya mrengo wa Muqawama katika eneo la Asia Magharibi yamelaani vikali jinai mpya ya kuogofya ya utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukanda wa Gaza, ambapo zaidi ya Wapalestina 100 wameuawa shahidi na makumi ya wengine kujeruhiwa.
-
Israel yaua Wapalestina zaidi ya mia moja na kujeruhiwa makumi kwenye eneo la ibada huko Gaza
Aug 10, 2024 04:00Zaidi ya Wapalestina 100 wameuawa shahidi na makumi ya wengine kujeruhiwa katika mauaji mapya yaliyofanywa na utawala vamizi wa Israel katikati mwa mji wa Gaza alfajiri ya leo, Jumamosi.
-
Pakistan yakanusha ripoti za Israel kuhusu kuipatia Iran silaha za nyuklia
Aug 10, 2024 03:56Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Pakistani, Mumtaz Zahra Baloch, amekanusha ripoti zilizochapishwa na vyombo vya habari vya Israel zinazodai kuwa Islamabad imejitolea kupeleka silaha za nyuklia nchini Iran, na kuzitaja ripoti hizo kuwa hazina msingi wowote.
-
Hali ngumu za watoto wa Gaza na bwabwaja za Wamagharibi
Aug 09, 2024 23:00Wakati Ripota Maalumu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Haki za Binadamu huko Palestina akitangaza kuwa mienendo isiyo ya kibinadamu ya utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya watoto wa Kipalestina ni jinai ya kivita, duru za Magharibi zinazodai kutetea haki za binadamu zinaendelea kunyamaza kimya mbele ya jinai hiyo na kukataa hata kuilaani kwa maneno tu.
-
UNICEF: Ghaza imegeuzwa makaburi ya watoto, hakuna mwisho wa mateso wanayopata
Aug 09, 2024 06:40Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Kuhudumia Watoto (UNICEF) umetangaza kuwa, Ukanda wa Ghaza umegeuzwa makaburi ya watoto wa Kipalestina na hakuna mwisho wa machungu na mateso wanayopata watoto hao.
-
Al-Houthi: Juhudi za Magharibi hazitazuia jibu la Iran kwa Israel
Aug 09, 2024 03:49Kiongozi wa Harakati ya Ansarullah ya Yemen amesisitiza kuwa, kucheleweshwa kwa jibu la mhimili wa Muqawama na Iran dhidi ya jinai na ukatili wa utawala wa Kizayuni ni suala la kimkakati ili kutoa nafasi ya kuligeuza kuwa jibu madhubuti.
-
Palestina yaitaka ICC kumkamata Smotrich baada ya kutoa wito wa kuuawa Wapalestina mil. 2 kwa njaa
Aug 08, 2024 23:19Wizara ya Mambo ya Nje ya Palestina imeitaka Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) kutoa hati ya kukamatwa Waziri wa Fedha wa Israel, Bezalel Smotrich, kwa sababu ya wito wake wa kuwaua kwa njaa Wapalestina milioni mbili huko Gaza.
-
Madhara na uharibifu wa kinyama unaofanywa na Wazayuni katika mauaji ya kimbari ya Wapalestina
Aug 08, 2024 23:16Utawala wa Kizayuni wa Israel haujajiwekea mipaka yoyote katika mauaji ya halaiki na ya kimbari unayofanya dhidi ya wananchi wa Palestina. Askari wenyewe wa jeshi la utawala huo dhalimu wamekuwa wakikiri waziwazi na bila ya hofu kwamba wanawaua makusudi Wapalestina wasio na ulinzi wa Ukanda wa Ghaza.
-
Gazeti la Kizayuni: Kiyama kitaishukia Israel kama Iran na Hizbullah zitashambulia kwa pamoja
Aug 08, 2024 07:11Gazeti moja la Kizayuni limetangaza kuwa, kiyama kitaishukia Israel iwapo Iran na Hizbullah zitaamua kufanya mashambulio ya pamoja dhidi ya utawala wa Kizayuni.