China, Tanzania na Zambia zasaini makubaliano mradi wa reli
Rais Xi-Jinping pamoja na Rais Samia Suluhu Hassan wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na mwenzao wa Zambia, Hakainde Hichilema wamesaini mkataba wa maelewano kuhusu mradi wa reli unaolenga kuimarisha mtandao wa usafiri wa reli na bahari.
Habari zaidii kutoka Beijing zinasema, China, Jamhurii ya Muungano wa Tanzania na Zambia zimesaini makubaliano ya mwanzo kuhusu mradi wa reli unaolenga kuimarisha mtandao wa usafiri wa reli na bahari katika kanda ya Afrika Mashariki.
Rais Xi-Jinping pamoja na Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan na mwenzake wa Zambia, Hakainde Hichilema wamesaini mkataba huo wa maelewano mjini Beijing ambako viongozi hao wanashiriki mkutano wa ushirikiano kati ya China na Afrika ulioanza rasmi leo.
China imesema, iko tayari kuutazama mkutano huo kama fursa ya kupiga hatua mpya ya kufufua ushirikiano wa reli kati ya Tanzania na Zambia ili kuimarisha mtandao wa usafiri wa reli na bahari kwenye kanda hiyo.
Mwanzoni mwa mwaka huu Benki ya Dunia iliidhinisha dola milioni 270 za kusaidia kuimarisha usafiri wa reli kati ya mataifa hayo jirani ya Tanzania na Zambia kunyanyua biashara kwenye eneo hilo.
Mkutano wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCACA) uulianza rasmi leo huko China utajadili kwa kina ushirikiano mpya wa kiuchumi, maendeleo ya miundombinu na ushirikiano wa pande mbili. Waziri wa Mambo ya Nje wa China Wang Yi amesema kuharakisha mabadiliko kunaiingiza dunia katika kipindi kipya cha misukosuko na mabadiliko.