Kundi la watu wenye silaha latiwa mbaroni Bunia Kongo
https://parstoday.ir/sw/news/africa-i19612-kundi_la_watu_wenye_silaha_latiwa_mbaroni_bunia_kongo
Inspekta wa Polisi katika mkoa wa Ituri nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ameripoti kutiwa mbaroni kundi moja la watu wenye silaha katika mji wa Bunia nchini humo.
(last modified 2023-11-27T08:44:11+00:00 )
Nov 17, 2016 00:54 UTC
  • Kundi la watu wenye silaha latiwa mbaroni Bunia Kongo

Inspekta wa Polisi katika mkoa wa Ituri nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ameripoti kutiwa mbaroni kundi moja la watu wenye silaha katika mji wa Bunia nchini humo.

Joseph Alimasi Inspekta wa Polisi katika mkoa wa Ituri ametangaza kuwa kundi hilo lililokamatwa la watu 20 limepelekea kuhitimishwa mauaji katika mji wa Bunia makao makuu ya mkoa wa Ituri. Alimasi ameongeza kuwa askari usalama juzi Jumanne waliwaarifisha watu hao kwa Jefferson Abdallah Penembaka Gavana wa mkoa wa Ituri. Inspekta wa polisi wa mkoa wa Ituri amepongeza hatua hiyo ya askari usalama wa huko Bunia na kuwatolea wito wakazi wa mji huo kuendeleza ushirikiano kati yao na polisi.

Mji wa Bunia makao makuu ya mkoa wa Ituri huko Kongo DR

Hii ni katika hali ambayo baadhi ya wakuu wa taasisi za kiraia huko Kongo wamesema wana wasiwasi na kuwepo makundi ya watu wenye silaha katika mji wa Bunia. Maeneo ya mashariki na kaskazini mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo yanakabiliwa na ukosefu wa amani kwa miaka 20 sasa.