Wapinzani S/Kusini wakaribisha mazungumzo ya kitaifa
https://parstoday.ir/sw/news/africa-i21544-wapinzani_s_kusini_wakaribisha_mazungumzo_ya_kitaifa
Wapinzani wa serikali ya Sudan Kusini wameunga mkono kufanyika mazungumzo ya kitaifa nchini humo.
(last modified 2023-11-27T08:44:11+00:00 )
Dec 16, 2016 12:05 UTC
  • Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini
    Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini

Wapinzani wa serikali ya Sudan Kusini wameunga mkono kufanyika mazungumzo ya kitaifa nchini humo.

Wapinzani hao wa serikali ya Juba leo wameunga mkono ombi la Rais Salva Kiir wa nchi hiyo la kutaka kufanyika mazungumzo ya kitaifa ili kurejesha amani, hata hivyo wameondoa uwezekano wa Kiir kushiriki kwenye mazungumzo hayo.

Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini juzi alitoa mwito wa kuanza mazungumzo ya kitaifa kwa kuyashirikisha makundi yote ya nchi hiyo.

Wanawake wa Sudan Kusini ambao wamekuwa wahanga wa udhalilishaji wa kijinsia 

Sudan Kusini ilitumbukia katika mzozo wa ndani na mgogoro wa kisasa tangu mwaka 2013 uliotokana na mapigano kati ya wafuasi wa Rais Salva Kiir na aliyekuwa Makamu wake Riek Machar.

Hali hiyo ya machafuko iliandaa uwanja wa kufanyika vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia, ubakaji na uhalifu mwingine dhidi ya wanawake huko Sudan Kusini bila ya wahusika kufikishwa katika vyombo vya sheria.