Russia: Uingiliaji kijeshi Libya unahitaji idhini ya Umoja wa Mataifa
Sergei Lavrov, Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia amesema leo Jumatatu kuwa uingiliaji kijeshi huko Libya unawezekana iwapo tu Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa litaidhinisha suala hilo.
Lavrov ameyasema hayo baada ya mazungumzo yake na Waziri mwenzake wa Tunisia huko Moscow kama ninavyomnukuu” tunafahamu kuhusu mipango ya uingiliaji kijeshi, ikiwemo hali ya mambo huko Libya. Mtazamo wetu wa pamoja ni huu kwamba uingiliaji huo unawezekana tu kwa kibali cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa,” mwisho wa kumnukuu.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia amesema oparesheni yoyote inayoweza kutekelezwa dhidi ya magaidi huko Libya ni lazima ibainishwe bila ya utata ili kuzuia tafsiri za uwongo na zenye kupotosha.