Maporomoko ya udongo yauwa watu 18 Rwanda, mvua kali zinaendelea kunyesha
https://parstoday.ir/sw/news/africa-i44178-maporomoko_ya_udongo_yauwa_watu_18_rwanda_mvua_kali_zinaendelea_kunyesha
Maporomoko ya udongo yaliyosababishwa na mvua kubwa yameuwa watu 18 katika mikoa ya kaskazini na magharibi mwa Rwanda mwishoni mwa wiki na kuifanya idadi ya watu walioaga dunia tangu mwezi Januari mwaka huu kutokana na mvua kali nchini humo kuwa zaidi ya 200.
(last modified 2023-11-27T08:44:11+00:00 )
May 07, 2018 10:55 UTC
  • Maporomoko ya udongo yauwa watu 18 Rwanda, mvua kali zinaendelea kunyesha

Maporomoko ya udongo yaliyosababishwa na mvua kubwa yameuwa watu 18 katika mikoa ya kaskazini na magharibi mwa Rwanda mwishoni mwa wiki na kuifanya idadi ya watu walioaga dunia tangu mwezi Januari mwaka huu kutokana na mvua kali nchini humo kuwa zaidi ya 200.

Philippe Habinshuti, Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma na Hatua za Dharura katika Wizara ya Kushughulikia Maafa na Wakimbizi ya Rwanda amesema leo kuwa mvua kubwa zilizonyesha usiku wa jana kuamkia leo zimeuwa watu 15 katika mikoa ya magharibi na kaskazini mwa nchi hiyo.

Phililippe Habinshuti, Afisa wa Kitengo cha Maafa na Huduma za Dharura wa Rwanda 

Habinshuti ameongeza kuwa miezi minne ya karibuni imekuwa mibaya zaidi kuliko kipindi cha mwaka jana na miaka mingine iliyopita.  Aidha watu watatu waliaga dunia mapema jana wilayani Rubavu nchini Rwanda.

Leo Jumatatu watu wamekuwa wakijaribu kuchimbua udongo wa matope kuwatafuta watu waliotoweka huko magharibi mwa Rwanda ambapo watu watatu hawajulikani waliko hadi sasa na sita wamejeruhiwa.