Katibu Mkuu UN asikitishwa na hali ya mambo Libya
https://parstoday.ir/sw/news/africa-i52660-katibu_mkuu_un_asikitishwa_na_hali_ya_mambo_libya
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametembelea Libya na kusema anaondoka nchini humo akiwa na hofu na moyo mzito.
(last modified 2026-03-21T11:32:05+00:00 )
Apr 06, 2019 04:08 UTC
  • Katibu Mkuu UN asikitishwa na hali ya mambo Libya

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametembelea Libya na kusema anaondoka nchini humo akiwa na hofu na moyo mzito.

Bwana Guterres ambaye alikuwepo ziarani Libya ambapo kwanza alitembelea mji mkuu Tripoli Alhamisi na kisha mji wa Bneghazi Ijumaa amesiktishwa sana vita vya ndani katika nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika. Akiwa Benghaziamekutana na Khalifa Haftar, kamanda wa wapiganaji wanaojiita Jeshi la kitaifa la Libya na kusistiza kuwa amani ya Libya itapatikana kwa njia ya mazungumzo na si vinginevyo.

Katibu Mkuu amewaambia waandishi wa habari baada ya mazungumzo hayo kuwa bado anaamini kuna uwezekano wa kuepusha umwagaji damu na mizozo kwenye mji mkuu Tripoli na viunga vyake.

Wapiganaji wa Haftar nchini Libya

 

Hata hivyo amesema, “Umoja wa Mataifa unasalia tayari kufanikisha suluhu yoyote ya kisiasa yenye lengo la kuungainsha taasisi za Libya. Chochote kitakachotokea, Umoja wa Mataifa bado umejizatiti kusaidia wananchi wa Libya. Walibya wana haki ya kupata amani, usalama, ustawi na haki zao za binadamu ziheshimiwe.”

Akiwa akiwa Tripoli, Katibu Mkuu alisisitiza kuwa Umoja wa Mataifa hauna ajenda binafsi wala maslahi kuhusu Libya isipokuwa ustawi wa watu wa Libya, amani na uwezekano wa kuishi katika demokrasia ya kawaida na wananchi kufaidika na utajiri mkubwa wa nchi.